-
“Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
2 Kwa kweli, mifano yenye matokeo haisahauliki upesi. Mwandikaji mmoja alisema kwamba mifano “hugeuza masikio kuwa macho” na kwamba “huwawezesha wasikilizaji kupiga picha akilini.” Kwa kuwa tunafahamu mambo vizuri zaidi tunapopiga picha akilini, mifano inaweza kufanya iwe rahisi zaidi kuelewa hata mambo yasiyoonekana kwa macho. Mifano inaweza kutusaidia kuwazia kinachozungumziwa na kufanya mafundisho yadumu akilini.
-
-
“Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
Kwa Nini Yesu Alitumia Mifano?
4, 5. Kwa nini Yesu alitumia mifano?
4 Biblia inaonyesha sababu mbili kuu zilizomfanya Yesu atumie mifano. Kwanza, kwa kufanya hivyo alitimiza unabii. Tunasoma hivi katika Mathayo 13:34, 35: “Yesu aliuambia umati mambo yote hayo kwa mifano. Kwa kweli, hakuwa akisema nao bila mfano; ili litimizwe lililosemwa kupitia nabii aliyesema: ‘Nitakifungua kinywa changu kwa mifano.’” Nabii aliyetajwa na Mathayo ni mwandikaji wa Zaburi 78:2. Mtunga-zaburi huyo aliandika maneno hayo kwa kuongozwa na roho ya Mungu mamia ya miaka kabla ya Yesu kuzaliwa. Fikiria jambo hilo. Miaka mingi mapema, Yehova alitabiri kwamba Masihi angefundisha kwa mifano. Hivyo basi, haikosi Yehova anathamini njia hii ya kufundisha.
5 Pili, Yesu alisema kwamba alitumia mifano kutenganisha watu ambao moyo wao “umekuwa mgumu.” (Mathayo 13:10-15; Isaya 6:9, 10) Mifano ya Yesu ilifunua nia za watu jinsi gani? Katika visa fulani, alitaka wasikilizaji wake wamwombe awafafanulie mifano ili waelewe maana kamili ya maneno yake. Watu wanyenyekevu walikuwa tayari kuuliza maswali lakini wenye kiburi au wasiopendezwa hawakutaka. (Mathayo 13:36; Marko 4:34) Basi, mifano ya Yesu iliwafunulia kweli wale ambao walitamani kutoka moyoni kuzijua; na wakati huohuo mifano yake iliwaficha wenye kiburi ile kweli.
6. Mifano ya Yesu ilitimiza makusudi gani yenye faida?
6 Mifano ya Yesu ilitimiza makusudi mengine yenye faida. Iliamsha upendezi kwa kuwachochea watu kusikiliza. Iliwawezesha kupiga picha akilini na kuzielewa kwa urahisi. Kama ilivyotajwa mwanzoni, mifano ya Yesu iliwasaidia wasikilizaji wake kukumbuka maneno yake. Mahubiri ya Mlimani, yaliyo katika Mathayo 5:3–7:27, ni mfano mzuri unaoonyesha jinsi Yesu alivyotumia mifano mingi. Hesabu moja ilionyesha kwamba kuna mifano zaidi ya 50 katika mahubiri hayo. Kumbuka kwamba mahubiri hayo yanaweza kusomwa kwa sauti kwa dakika 20 hivi. Hivyo, kwa wastani, mfano unatajwa karibu kila sekunde 20! Ni wazi kwamba Yesu aliona faida ya kutokeza picha akilini!
-