Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Juni 15
    • 7 Fikiria mfano huu. Ikiwa rafiki yako angekuwa na kipawa cha pekee, labda katika michezo, sanaa, au muziki, je, ungewaeleza watu wa familia yenu na marafiki wengine kumhusu? Bila shaka. Kujifunza yote ambayo Yehova amefanya kunaweza pia kutuchochea kufanya vivyo hivyo. Kwa mfano, Zaburi 19:1, 2 inasema kwamba anga yenye nyota hufanya “maneno yabubujike.” Nasi tunapofikiria mambo ya ajabu ambayo Yehova amefanya, hatuwezi kuacha kuwaeleza wengine kumhusu Mungu wetu.

  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Juni 15
    • 10. Kwa nini tunachochewa kumsifu Mungu?

      10 Bado kuna sababu nyingine ya kumsifu Yehova. Kumbuka ule mfano wa rafiki yako mwenye kipawa cha pekee. Kama ungesikia wengine wakisema uwongo kumhusu na kuchongea jina lake, je, hungejitahidi hata zaidi kumsifu? Yehova amechongewa sana katika ulimwengu huu. (Yohana 8:44; Ufunuo 12:9) Hivyo, wale wanaompenda wanachochewa kusema kweli kumhusu. Je, wewe pia ungependa kudhihirisha upendo na shukrani zako kwa Yehova na kuonyesha kwamba unataka awe Mtawala wako badala ya kutawaliwa na Shetani, adui yake mkuu? Unaweza kufanya yote hayo kwa kumsifu Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki