-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Jamii ya kibinadamu ikazidi kuzama ndani ya tope la ukosefu wa adili kingono. Kupitia Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine pamoja na programu za mkusanyiko, watu wa Yehova waliimarishwa ili ‘kusimama imara katika imani’ wakati wa mwongo huo wa miaka wenye msukosuko.—1 Kor. 16:13.
-
-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mashahidi wa Yehova hawakuepuka kuathiriwa na mabadiliko ya maoni ya miaka ya 1960 juu ya ngono. Kwa kweli, maelfu kadhaa—asilimia ndogo ya idadi yao yote—walilazimika kutengwa na ushirika kila mwaka, walio wengi wao kwa sababu ya ukosefu wa adili kingono. Basi, kukiwa na sababu nzuri, watu wa Yehova walipewa shauri la moja kwa moja kwenye mfululizo wa mikusanyiko iliyofanywa katika 1964. Lyle Reusch, mwangalizi asafiriye aliyetoka hapo kwanza Saskatchewan, Kanada, alikumbuka hotuba “Kuendeleza Tengenezo la Watumishi wa Umma Likiwa Limetakata, Safi.” Reusch akasema hivi: “Lugha yenye kutaja mambo waziwazi, kikweli, juu ya maadili ilieleza mambo waziwazi kwa usemi ulio wazi.”
Yaliyokuwamo katika hotuba hiyo yalitangazwa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza), la Novemba 15, 1964. Miongoni mwa mambo mengine, liliarifu hivi: “Wasichana, msijifanye wenyewe kuwa taulo chafu kwa matumizi ya umma, mkipatikana ili mtumiwe na mikono michafu ya mfanya-umalaya yeyote, ‘mbwa’ yeyote wa ufananisho.”—Linganisha Ufunuo 22:15.
Shauri hilo lenye kutaja mambo waziwazi lilikusudiwa kusaidia Mashahidi wa Yehova wakiwa kikundi cha watu ili wakae wakiwa katika hali safi kiadili, wenye kufaa kuendelea kupiga mbiu ya ujumbe wa Ufalme.—Linganisha Warumi 2:21-23.
-