-
Wasaidieni Warudi Haraka!Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
18 Ndugu huyo alipokewa jinsi gani katika kutaniko? Anasema hivi: “Ninahisi kama yule mwana mpotevu aliyetajwa na Yesu Kristo. Kwa hakika, dada mmoja mwenye umri mkubwa ambaye alikuwapo miaka 30 iliyopita na ambaye bado anamtumikia Yehova kwa uaminifu aliniambia, ‘Mwanangu, karibu nyumbani!’ Hilo lilinigusa moyo sana. Kwa kweli, nilikuwa nimerudi nyumbani. Ningependa kumshukuru kutoka moyoni mzee huyo na kutaniko lote kwa sababu ya kunionyesha upendo, uchangamfu, subira, na kunijali. Upendo wao kwa Yehova na jirani ulinisaidia kwelikweli kurudi katika kundi.”
-
-
Wasaidieni Warudi Haraka!Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
21, 22. Unaweza kuwahakikishia nini wale wanaomrudia Yehova?
21 Ikiwa kondoo aliyeacha kushirikiana na kundi anaogopa kukutana tena na ndugu zake, unaweza kumkumbusha jinsi watu walivyoshangilia wakati mwana mpotevu aliporudi nyumbani. Wale wanaorudi katika kutaniko wanawachochea wengine kuwa na shangwe kama hiyo. Watie moyo wachukue hatua sasa ya kumpinga Ibilisi na kumkaribia Mungu.—Yak. 4:7, 8.
22 Wale wanaomrudia Yehova watakaribishwa kwa shangwe. (Omb. 3:40)
-