-
Nilikuwa Kiongozi wa Dini ya WakickapooAmkeni!—2004 | Novemba 8
-
-
Dini ya Peyote
Dini ya Peyote imeenea katika makabila mengi ya Wahindi leo. Quanah Parker (1845-1911 hivi), kiongozi wa dini na chifu wa ukoo wa Kwahadi wa kabila la Comanche, “alihusika sana katika kuendeleza dini ya peyote katika Eneo la Wahindi.” (The Encyclopedia of Native American Religions) Alitangaza kwa bidii ubora wa dawa za kulevya za mmea wa dungusi aina ya peyote unaosemekana una uwezo wa kuponya. Alipata wafuasi katika makabila mengi ya Wahindi wa Amerika Kaskazini. Kwa hiyo, miongoni mwa Wakickapoo, kama vile makabila mengine mengi, dini mbili zilikubaliwa, yaani, dini yao ya kikabila na vilevile dini ya Peyote.
-
-
Nilikuwa Kiongozi wa Dini ya WakickapooAmkeni!—2004 | Novemba 8
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 22]
Dini ya Peyote Ni Nini?
Sasa, dini ya Peyote inaitwa Kanisa la Wahindi wa Amerika. Peyote ni mmea mdogo aina ya dungusi (ona kulia) unaopatikana hasa katika bonde la Rio Grande huko Mexico na pia Texas. Dini ya Peyote ina zaidi ya wafuasi 200,000 wa makabila ya Amerika Kaskazini. “Leo, dini hiyo ambayo ilianzishwa zamani huko Mexico, inahusisha mambo ya Ukristo, lakini bado ni dini ya Wahindi pekee.” (A Native American Encyclopedia—History, Culture, and Peoples) Sherehe ya Mwezi-Nusu na ya Mwezi Mkubwa ndizo muhimu zaidi katika dini ya Peyote. Sherehe hizo zinahusisha “utamaduni wa Kihindi na Ukristo.” Sherehe hizo ambazo kwa kawaida huanza Jumamosi, husherehekewa usiku kucha. Wakati wa sherehe hizo kikundi cha wanaume huketi kwa mviringo ndani ya hema lenye umbo la pia. Wao hupata maono huku wakila chipukizi nyingi chungu za dungusi ya peyote, na kuimba nyimbo takatifu kwa kufuatana na mdundo wa ngoma na kibuyu chenye kulia kama kayamba.
[Hisani]
Courtesy TAMU Cactus Photo Gallery
-