-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Wenye Nia Kutumika Kokote Kulikokuwa na Uhitaji
Tamaa yao ya moyoni ya kufanya kazi ambayo Yesu alikuwa amewagawia wanafunzi wake iliwaongoza wafanyakazi hao wa wakati wote kwenye maeneo mapya, hata kwa nchi mpya. Frank Rice alipoalikwa aondoke Australia ili akafungue kazi ya kuhubiri habari njema katika Java (sasa ni sehemu ya Indonesia) katika 1931, alikuwa amepata ujuzi wa miaka kumi katika huduma ya wakati wote. Lakini sasa kulikuwa na desturi mpya, kutia na lugha mpya za kujifunza. Angeweza kutumia Kiingereza kutoa ushahidi kwa wengine madukani au maofisini, lakini alitaka kutolea wengine ushahidi pia. Yeye alijifunza kwa bidii, na katika miezi mitatu alijua Kiholanzi cha kutosha kuanza kwenda nyumba hadi nyumba. Kisha akajifunza Kimaleya.
Frank alikuwa na miaka 26 tu alipoenda Java, na kwa sehemu kubwa ya miaka sita aliyokuwa huko na Sumatra, alifanya kazi akiwa peke yake. (Kuelekea mwisho wa 1931, Clem Deschamp na Bill Hunter walikuja kutoka Australia ili kusaidia kazi. Wakiwa kikundi, walifanya ziara ya kuhubiri kuelekea bara, huku Frank akifanya kazi katika jiji kuu la Java. Baadaye, Clem na Bill pia walipokea migawo iliyowapeleka sehemu nyinginezo.) Hakukuwa na mikutano ya kutaniko ambayo Frank angeweza kuhudhuria. Nyakati nyingine alikuwa mpweke sana, na mara kadhaa alishindana na mawazo ya kuacha na kurudi Australia. Lakini aliendelea tu. Jinsi gani? Chakula cha kiroho kilichomo katika The Watch Tower kilimtia nguvu. Katika 1937 alienda kwenye mgawo katika Indochina, ambapo alinusurika kufa wakati wa misukosuko ya jeuri iliyofuata Vita ya Ulimwengu 2. Roho hiyo ya kutaka kutumikia ilikuwa ingali hai katika miaka ya 1970 alipoandika ili kuonyesha shangwe yake kwa sababu familia yake yote ilikuwa ikimtumikia Yehova na kusema kwamba yeye na mke wake walikuwa wakijitayarisha tena kuhamia sehemu fulani katika Australia kulikokuwa na uhitaji mkubwa zaidi.
-
-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 287]
Frank Rice (anayesimama upande wa kulia), Clem Deschamp (aliyeketi mbele ya Frank, pamoja na mke wa Clem, Jean, kando yao), na kikundi katika Java kutia na Mashahidi wenzi na watu waliopendezwa karibuni
-