Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kulinda Familia Yako Dhidi ya Homa
    Amkeni!—2010 | Juni
    • Njia za Kujikinga

      Serikali nyingi zimetambua umuhimu wa kujitayarisha kwa ajili ya milipuko ya homa. Lakini wewe unaweza kufanya nini? Acheni tuchunguze hatua tatu za msingi za kujikinga:

      Imarisha mwili wako: Hakikisha kuwa familia yako inapata usingizi wa kutosha na kula vyakula vitakavyosaidia mwili kuimarisha kinga yake. Hakikisha kwamba unakula matunda, mboga, nafaka, na protini zisizo na mafuta mengi ambazo zitakupa asidi amino zinazohitajika ili kuimarisha mfumo wako wa kinga.

      Usiruhusu viini nyumbani: Kwa kadiri unavyoweza, hakikisha kwamba meza ni safi kabisa kila siku. Osha vyombo vya kupikia na vya kula baada ya kuvitumia na uoshe matandiko kwa ukawaida. Tumia sabuni ya kuua viini kupangusa vitu ambavyo watu hugusa kama vile: mlango, simu, kifaa cha televisheni cha kubonyeza kutoka mbali. Ikiwezekana, hakikisha kuna hewa safi ya kutosha.

      Dumisha mazoea mazuri ya usafi: Osha mikono yako vizuri kwa sabuni na maji. (Ikiwa inafaa, beba chupa ndogo yenye sabuni ya kuua viini.) Ikiwezekana, usitumie taulo moja kukausha mikono au uso pamoja na mtu mwingine yeyote kutia ndani hata watu wa familia.

      Usiguse macho, mapua, au mdomo bila kunawa mikono. Ikiwezekana, tumia shashi kufunika mdomo na mapua unapokohoa au kupiga chafya na uitupe mara moja. Epuka kutumia vifaa pamoja na wengine vinavyoweza kueneza viini, kama vile simu. Watoto wanahitaji kuzoezwa kabisa kuhusu mambo hayo. Mazoea hayo yanafaa kila wakati lakini yanafaa zaidi wakati watu wengi wana homa.

      Wajali Watu Wengine

      Unaweza kuambukiza wengine siku moja kabla ya dalili za homa kuonekana na siku tano baada ya kuugua. Dalili hizo zinafanana na zile za mafua lakini zinamwathiri mtu zaidi. Zinatia ndani kuongezeka sana kwa joto mwilini, maumivu ya kichwa, kuchoka sana, kohozi kavu, na maumivu ya misuli. Kutokwa na kamasi na matatizo ya tumbo—kama vile kichefuchefu, kutapika, na kuendesha—huwaathiri watoto zaidi kuliko watu wazima. Ikiwezekana, ukiwa na dalili hizo kaa nyumbani ili usiwaambukize wengine.

  • Kulinda Familia Yako Dhidi ya Homa
    Amkeni!—2010 | Juni
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 28, 29]

      NJIA 6 ZA KUJILINDA NA KUWALINDA WENGINE

      1. Funika kinywa unapokohoa

      2. Nawa mikono

      3. Hakikisha nyumba ina hewa safi ya kutosha

      4. Dumisha usafi

      5. Ukiwa mgonjwa, usitoke nyumbani

      6. Epuka kuwagusa wengine

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki