-
Je, Wewe Una “Uhuru wa Kusema”?Mnara wa Mlinzi—2006 | Mei 15
-
-
Sala ilimsaidia Sherry kuwa na ujasiri wa kutoa ushahidi nafasi ilipojitokeza. Siku moja alipokuwa akimsubiri mume wake arudi kutoka katika shughuli fulani, alimwona mwanamke mwingine akiwa anasubiri pia. “Nikiwa na wasiwasi mwingi,” asema Sherry, “nilimwomba Yehova anipe ujasiri.” Sherry alipomkaribia mwanamke huyo, kasisi Mbaptisti akafika. Sherry hakutarajia kukutana na kasisi. Hata hivyo, alisali tena naye akapata ujasiri wa kutoa ushahidi. Alimwachia mwanamke huyo vichapo na kupanga ziara ya kurudia. Tunapotumia nafasi zinazojitokeza ili kutoa ushahidi, tunaweza kuwa na hakika kwamba kumtegemea Yehova kutatusaidia kusema kwa uhuru.
-
-
Je, Wewe Una “Uhuru wa Kusema”?Mnara wa Mlinzi—2006 | Mei 15
-
-
Ili kufundisha kwa matokeo, Wakristo wote wanahitaji kuwa na uhuru wa kusema. Sherry, aliyetajwa awali, alitaka kuwatia moyo watoto wake watoe ushahidi shuleni. “Hata ingawa nililelewa katika kweli,” anakiri, “sikuwa na mazoea ya kutoa ushahidi shuleni. Na kwa kawaida sihubiri isivyo rasmi. Nilijiuliza hivi, ‘Ni kielelezo cha aina gani ninachowawekea watoto wangu?’” Jambo hilo lilimchochea Sherry kujitahidi zaidi kuhubiri isivyo rasmi.
-