Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kuhubiri Isivyo Rasmi!
    Huduma ya Ufalme—2010 | Agosti
    • 3. Ni nini kinachoweza kutusaidia ikiwa sisi ni wenye haya?

      3 Jinsi ya Kuanza: Wengi wetu huona ikiwa vigumu kuanzisha mazungumzo na watu tusiowajua. Hata huenda ikawa vigumu kuwahubiria watu tunaowajua. Hata hivyo, tutachochewa kuwahubiria ikiwa tutatafakari wema wa Yehova, hazina za kiroho ambazo amewapa watumishi wake, na hali mbaya ambazo watu wanakabiliana nazo katika ulimwengu. (Yona 4:11; Zab. 40:5; Mt. 13:52) Zaidi ya hayo, tunaweza kumwomba Yehova atusaidie ‘kujipa ujasiri.’ (1 The. 2:2) Mwanafunzi mmoja wa Shule ya Gileadi alisema: “Nimetambua kwamba sala inasaidia wakati ambapo ni vigumu kwangu kuzungumza na watu.” Ikiwa unasita kusema, toa sala fupi ya kimyakimya.—Neh. 2:4.

      4. Tunaweza kujitahidi kufanya nini mwanzoni, na kwa nini?

      4 Tunapohubiri isivyo rasmi, hatuhitaji kuanza mazungumzo kwa njia rasmi au kwa kusoma andiko kama tunavyofanya tunapohubiri nyakati nyingine. Linaweza kuwa jambo bora kujitahidi kuanzisha mazungumzo bila kuhisi kwamba ni lazima tuhubiri moja kwa moja. Wahubiri wengi wanasema kwamba kwa kufanya hivyo wanapata ujasiri wa kuwaambia watu kuhusu habari njema hatimaye. Ikiwa mtu hataki mazungumzo, hakuna haja ya kumlazimisha azungumze nawe. Malizia mazungumzo kwa upole na uendelee na shughuli zako.

      5. Ni nini ambacho humsaidia dada mmoja mwenye haya kuhubiri isivyo rasmi?

      5 Dada mmoja mwenye haya huanza kwa kumtazama mtu na kutabasamu anapokuwa akinunua vitu sokoni. Mtu huyo anapotabasamu pia, dada huyo husema maneno machache. Ikiwa mtu huyo anaitikia vema, dada huyo hupata ujasiri wa kuendeleza mazungumzo. Dada huyo husikiliza kwa makini na kujaribu kujua ni ujumbe gani unaomfaa mtu huyo. Kwa kufanya hivyo, amewapa watu vichapo vingi na hata ameanzisha funzo la Biblia.

      6. Tunaweza kuanzishaje mazungumzo yasiyo rasmi?

      6 Kuanzisha Mazungumzo: Tunaweza kufanya nini ili kuanzisha mazungumzo? Yesu alipozungumza na mwanamke fulani katika kisima, alianza kwa kumwomba maji tu. (Yoh. 4:7) Kwa hiyo, tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa salamu za kirafiki au kuuliza swali. Mnapoongea, unaweza kupata nafasi ya kutoa wazo la Kimaandiko na labda upande mbegu ya kweli. (Mhu. 11:6) Wengi wamefanikiwa kwa kusema maneno yenye kuamsha fikira ambayo huwafanya wengine watake kupata habari zaidi. Kwa mfano, unaposubiri kumwona daktari, unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema, “Nitafurahi sana wakati ambapo sitakuwa mgonjwa tena.”

      7. Kuwa watambuzi kunaweza kutusaidiaje kuhubiri isivyo rasmi?

      7 Kuwa watambuzi kutatusaidia pia kuanzisha mazungumzo. Tunapomwona mzazi aliye na watoto wenye tabia nzuri, tunaweza kumpongeza na kumwuliza, “Ni nini ambacho kimekusaidia kufanikiwa kuwa mzazi mzuri?” Dada mmoja husikiliza mambo ambayo wafanyakazi wenzake huzungumzia na kisha kutayarisha ujumbe wake kulingana na mambo yanayowapendeza. Alipojua kwamba mwanamke fulani kazini alikuwa akipanga harusi, alimpa nakala ya gazeti la Amkeni! iliyohusu jinsi ya kupanga harusi. Jambo hilo liliongoza kwa mazungumzo zaidi ya Biblia.

      8. Tunaweza kutumiaje vitabu vyetu kuanzisha mazungumzo?

      8 Njia nyingine ya kuanzisha mazungumzo ni kwa kusoma vitabu vyetu tunapokuwa mahali ambapo wengine wanaweza kutuona. Ndugu mmoja hufungua makala inayovutia katika gazeti la Mnara wa Mlinzi au Amkeni! na kuanza kusoma. Anapotambua kwamba mtu aliye karibu anatazama gazeti hilo, yeye huuliza swali au kutoa maelezo mafupi kuhusu makala anayosoma. Mara nyingi hilo humwezesha kuanzisha mazungumzo na kutoa ushahidi. Kuacha kimojawapo ya vitabu vyetu mahali ambapo watu wanaweza kukiona, kunaweza kuwachochea wafanyakazi au wanafunzi wenzetu kuuliza maswali kukihusu.

  • Unaweza Kuhubiri Isivyo Rasmi!
    Huduma ya Ufalme—2010 | Agosti
    • [Sanduku katika ukurasa wa 5]

      Madokezo ya Kuanzisha Mazungumzo

      ◼ Mwombe Yehova akusaidie ili uanzishe mazungumzo

      ◼ Tafuta watu wanaoonekana kuwa wenye urafiki na wasio na haraka

      ◼ Watazame, utabasamu, na useme maneno machache ya mambo ambayo mnaweza kukubaliana

      ◼ Wasikilize vizuri wanapoongea

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki