-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
Waandikaji fulani wa Biblia walishiriki katika utafiti kwa kadiri kubwa ili kuandika habari zao. Kwa kielelezo, Luka, aliandika hivi kwa habari ya simulizi lake la Gospeli: “Nimefuatisha kwa uangalifu mambo yote tangu awali kwa usahihi, [kuandikia] hayo kwa utaratibu wenye kufuatana vizuri.” Bila shaka, roho ya Mungu ilibariki jitihada za Luka, pasipo shaka ikimsukuma kupata hati za kihistoria zenye kuaminika na kuhoji mashahidi wa kujionea wenye kutegemeka, kama vile wanafunzi waliokuwa hai na yawezekana mama ya Yesu, Maria. Roho ya Mungu basi ingemwongoza Luka kurekodi hiyo habari kwa usahihi.—Luka 1:1-4.
-
-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
Katika visa fulani waandikaji wa Biblia walitia ndani mitungo kutoka kwenye hati zenye ushahidi wa kujionea za waandikaji wa kihistoria wa mapema zaidi, ambao si wote waliokuwa wamepuliziwa. Yeremia alitumia njia hiyo kwa kadiri kubwa kutunga kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Wafalme. (2 Wafalme 1:18) Ezra alirejezea angalau vyanzo 14 visivyopuliziwa ili kukusanya habari kwa ajili ya kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Mambo ya Nyakati, kutia ndani “taarifa za mfalme Daudi” na “kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.” (1 Mambo ya Nyakati 27:24; 2 Mambo ya Nyakati 16:11) Musa hata alinukuu kutoka “chuo [“kitabu,” NW] cha Vita vya BWANA”—yaonekana kilikuwa rekodi yenye kutegemeka ya vita vya watu wa Mungu.—Hesabu 21:14, 15.
Katika visa hivyo roho takatifu ilihusika kiutendaji, ikisukuma waandikaji wa Biblia kuteua habari zenye kutegemeka, ambazo wakati huo zilipata kuwa sehemu ya rekodi ya Biblia iliyopuliziwa.
-