-
Sifa ya Kutumainika Katika Ulimwengu Usio MkamilifuMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
Mfalme Daudi wa Israeli alifanya makosa mengi, kutia ndani uhusiano wake wenye uzinzi pamoja na Bath-sheba, wenye uthibitisho wa kutosha. (2 Samweli 11:1-27) Makosa mengi ya Daudi yalithibitisha kwamba hakuwa mkamilifu hata kidogo. Lakini, ni nini Yehova alichoona katika huyo mtu? Akizungumza na Solomoni, mwana wa Daudi, Yehova alisema hivi: “Tembea mbele yangu, sawa tu na vile Daudi baba yako alivyotembea, kwa uaminifu-maadili wa moyo na unyoofu.” (1 Wafalme 9:4, NW) Yajapokuwa makosa yake mengi, kutumainika kwa msingi, kwa Daudi, kulitambuliwa na Yehova. Kwa nini?
Daudi alitoa jibu alipomwambia Solomoni hivi: “BWANA hutafuta-tafuta mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira.” (1 Mambo ya Nyakati 28:9) Daudi alifanya makosa, lakini alikuwa mnyenyekevu, naye alitaka kufanya lililo sawa. Sikuzote alikubali karipio na usahihisho—kwa kweli, aliomba kusahihishwa. “Unijaribu na kunipima; unisafishe mtima wangu na moyo wangu” ndivyo alivyoomba. (Zaburi 26:2) Na bila shaka Daudi alisafishwa. Kwa kielelezo, masharti yaliyotokana na dhambi yake pamoja na Bath-sheba, yalidumu hadi mwisho wa uhai wake. Bado, Daudi hakujaribu kamwe kutetea kosa lake. (2 Samweli 12:1-12) La maana zaidi, hakuenda kamwe upande kutoka ibada ya kweli. Kwa sababu hiyo, na kwa sababu ya majuto na toba ya kweli ya Daudi, yenye kuhisiwa moyoni, Yehova alikuwa tayari kusamehe dhambi zake na kumkubali kuwa mtu mwenye uaminifu-maadili.—Ona pia Zaburi 51.
-
-
Sifa ya Kutumainika Katika Ulimwengu Usio MkamilifuMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
Mtu mwenye uaminifu-maadili aweza kutumainiwa, si na mwanadamu mwenzake tu, bali pia la maana zaidi, aweza kutumainiwa na Mungu. Usafi wake wa moyo unaonwa katika matendo yake; yeye hana unafiki. Si mwenye vipengee wala si mfisadi. Mtume Paulo alieleza hilo hivi: “Tumeyakataa kabisa mambo ya kichinichini yaliyo ya kuaibikia, si kutembea kwa ujanja, wala tukilighushi neno la Mungu, bali kwa kufanya kweli iwe dhahiri tukijipendekeza wenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu machoni pa Mungu.”—2 Wakorintho 4:2.
-