-
Utangulizi Unaoamsha UpendeziFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Unapokuwa katika utumishi wa shambani, pia unahitaji kuvuta usikivu wa watu. Ikiwa hamkupanga kukutana, huenda ikawa mwenye nyumba ana shughuli nyingi. Katika sehemu fulani za ulimwengu, wageni wasiotarajiwa wanapaswa kutaja haraka kilichowaleta. Na katika sehemu nyinginezo, watu hufuata desturi ya kujuliana hali kabla ya kusema kilichowaleta.—Luka 10:5.
Kwa vyovyote vile, urafiki wa kweli unaweza kutokeza mazingira mazuri ya mazungumzo. Mara nyingi inafaa kuanza na jambo ambalo linamhusu mtu huyo. Unaweza kulitambuaje? Umemkuta akifanya nini? Labda analima, anatunza ua wa nyumba, anarekebisha gari, anapika, anafua, au anawashughulikia watoto. Je, kuna kitu anachotazama—gazeti fulani au tukio fulani barabarani? Je, kuna dalili nyumbani kwake kwamba anapenda kuvua samaki, michezo, muziki, kusafiri, kompyuta, au jambo jingine lolote? Mara nyingi, watu huhangaikia habari za redio au za televisheni. Swali fulani au jambo fupi kuhusu habari kama hizo linaweza kutokeza mazungumzo ya kirafiki.
Pindi ambapo Yesu alizungumza na yule mwanamke Msamaria kwenye kisima fulani karibu na Sikari ni mfano bora wa jinsi ya kuanzisha mazungumzo ili kuhubiri.—Yn. 4:5-26.
Unahitaji kutayarisha utangulizi kwa makini, hasa ikiwa eneo la kutaniko lenu linahubiriwa mara nyingi. Usipofanya hivyo, unaweza kushindwa kuhubiri.
-
-
Utangulizi Unaoamsha UpendeziFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Yesu alipowatuma wanafunzi wake, alitaja wazi ujumbe ambao walipaswa kuhubiri. “Mwendapo, hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa mbingu umekaribia.’” (Mt. 10:7) Yesu alisema hivi kuhusu siku zetu: “Habari njema hii ya ufalme itahubiriwa.” (Mt. 24:14) Tunahimizwa ‘tuhubiri neno,’ yaani, tushikamane na Biblia tunapohubiri. (2 Tim. 4:2) Na mara nyingi ni vizuri kutaja jambo linalohangaisha watu wakati huo kabla ya kufungua Biblia au kabla ya kuzungumza juu ya Ufalme. Unaweza kutaja uhalifu, ukosefu wa kazi, ukosefu wa haki, vita, jinsi ya kuwasaidia vijana, ugonjwa, au kifo. Lakini usizungumzie matatizo kwa urefu kwa sababu una ujumbe unaotia moyo. Jaribu kuelekeza mazungumzo kwenye Neno la Mungu na tumaini la Ufalme.
-
-
Utangulizi Unaoamsha UpendeziFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Iwe unatoa hotuba jukwaani au unamhubiria mtu, mojawapo ya njia bora zaidi za kuamsha upendezi ni kuwahusisha wale wanaokusikiliza. Onyesha jinsi habari unayozungumzia inavyohusu matatizo yao, mahitaji yao, au maswali wanayofikiria. Ukionyesha wazi kwamba hutazungumza habari hiyo kwa ujumla bali utazungumzia mambo hususa, watakusikiliza kwa makini zaidi. Ni lazima utayarishe vizuri ili ufaulu.
-