-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Isaya—2Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 15
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Isaya—2
ISAYA alitimiza kwa uaminifu kazi yake akiwa nabii. Hukumu alizotangaza juu ya ufalme wa makabila kumi ya Israeli tayari zimetimia. Sasa ana ujumbe mwingine kuhusu wakati ujao wa Yerusalemu.
Jiji la Yerusalemu litaharibiwa, na wakaaji wake watachukuliwa mateka. Hata hivyo, uharibifu wake hautadumu. Baada ya muda, ibada ya kweli itarudishwa. Huo ndio ujumbe unaokaziwa hasa katika Isaya 36:1–66:24.a
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Isaya—2Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 15
-
-
“TAZAMA! SIKU ZINAKUJA”
Katika mwaka wa 14 wa utawala wa Mfalme Hezekia (732 K.W.K.), Waashuru wanashambulia Yuda. Yehova anaahidi kulinda jiji la Yerusalemu. Tisho la kushambuliwa linakoma wakati malaika mmoja tu wa Yehova anapowaua askari-jeshi 185,000 Waashuru.
Hezekia ni mgonjwa. Yehova anajibu sala yake na kumponya, naye anamwongezea miaka 15 ya maisha. Mfalme wa Babiloni anapotuma wajumbe wampongeze, Hezekia anakosa hekima na kuwaonyesha hazina zake zote. Isaya anamjulisha Hezekia ujumbe huu wa Yehova: “Tazama! Siku zinakuja, na vyote vilivyo ndani ya nyumba yako na ambavyo mababu zako wameweka akiba mpaka leo hii kwa kweli vitachukuliwa kwenda Babiloni.” (Isaya 39:5, 6) Baada ya miaka mia moja na kitu, unabii huo unatimia.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Isaya—2Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 15
-
-
“ATAJENGWA UPYA”
Mara tu baada ya kutabiri uharibifu wa Yerusalemu na Waisraeli kupelekwa utekwani huko Babiloni, Isaya anatabiri kuhusu kurudishwa kwa ibada ya kweli. (Isaya 40:1, 2) Andiko la Isaya 44:28 linasema: “[Yerusalemu] atajengwa upya.” Sanamu za miungu ya Babiloni zitabebwa kama “vifurushi.” (Isaya 46:1) Babiloni litaharibiwa. Yote hayo yanatimia baada ya karne mbili.
Yehova atamtoa mtumishi wake kuwa “nuru ya mataifa.” (Isaya 49:6) “Mbingu” au watawala wa Babiloni, “zitatawanywa vipande-vipande kama moshi,” na raia wake “watakufa kama chawa”; lakini ‘binti Sayuni aliye mateka atajifungua pingu za shingo yake.’ (Isaya 51:6; 52:2) Kwa wote ambao wanakuja kwake na kumsikiliza, Yehova anasema hivi: “Bila kusita mimi nitafanya pamoja nanyi agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo kuhusu fadhili zenye upendo kwa Daudi.” (Isaya 55:3) Kuishi kulingana na matakwa ya uadilifu ya Mungu kunaleta “furaha tele katika Yehova.” (Isaya 58:14) Kwa upande mwingine, makosa ya watu, ‘yanasababisha mgawanyiko kati yao na Mungu wao.’—Isaya 59:2.
-