Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • na kila mlima na kila kisiwa viliondolewa mahali pavyo.” (Ufunuo 6:14, NW) Kwa wazi hizi si mbingu halisi au milima na visiwa halisi. Lakini hizo zinafananisha nini?

  • Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 24. (a) Katika unabii wa Biblia, ni wakati gani inaposemwa kwamba milima na visiwa vinatikiswa au kuondolewa uimara? (b) ‘Milima ilitikisikaje’ wakati Ninawi ulipoanguka?

      24 Katika unabii wa Biblia, milima na visiwa vinasemwa kuwa vinatikiswa au kuondolewa uimara wakati wa mabadiliko makubwa ya kisiasa. Mathalani, wakati wa kutabiri hukumu za Yehova dhidi ya Ninawi, nabii Nahumu aliandika: “Milima yenyewe imetikisika kwa ajili ya yeye, na vilima halisi vikajikuta vyenyewe vikiyeyuka. Nayo dunia itapinduliwa kwa sababu ya uso wake.” (Nahumu 1:5, NW) Hakuna maandishi yanayoonyesha kuvunjika kokote kwa milima halisi wakati Ninawi ulipoanguka kikweli katika 632 K.W.K. Lakini serikali kubwa ya ulimwengu ambayo hapo kwanza ilionekana kuwa kama mlima katika imara yayo ilianguka ghafula.—Linga Yeremia 4:24.

      25. Kwenye ule mwisho unaokuja wa huu mfumo wa mambo, “kila mlima na kila kisiwa” vitaondolewaje mahali pavyo?

      25 Kwa hiyo, kimantiki “kila mlima na kila kisiwa” kama inavyorejezewa mwanzoni mwa kufunguliwa kwa kifungo cha sita vingekuwa serikali za kisiasa na matengenezo yanayozitegemea ya ulimwengu huu ambazo zimeonekana kuwa imara sana kwa wengi wa aina ya binadamu. Zitatikiswa zitoke mahali pazo, kwa fadhaa na hofu ya wale ambao hapo kwanza waliziitibari. Kama vile unabii huo uendeleavyo kusimulia, hakutakuwa na shaka lolote kwamba ile siku kubwa ya hasira-kisasi ya Yehova na Mwana wake—lile tetemeko la mwisho kabisa ambalo linaondoa matengenezo yote ya Shetani—imekuja ikiwa na kisasi!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki