-
Muumba Ajifunua—Kwa Manufaa Yetu!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Muumba Ajifunua—Kwa Manufaa Yetu!
KATI ya ngurumo na radi, watu wapatao milioni tatu walisimama mbele ya mlima mrefu katika Peninsula ya Sinai. Mawingu yalifunika Mlima Sinai, ardhi ikatetemeka. Katika hali hizo zenye kukumbukwa, Musa aliongoza Israeli la kale kufanya agano pamoja na Muumba wa mbingu na dunia.—Kutoka, sura ya 19; Isaya 45:18.
Lakini, kwa nini Muumba wa ulimwengu angejifunua kwa njia ya kipekee kwa taifa moja tu, na isitoshe taifa dogo tu? Musa alitufahamisha hivi: ‘Kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.’—Kumbukumbu la Torati 7:6-8.
-
-
Muumba Ajifunua—Kwa Manufaa Yetu!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Yehova alimwahidi Abrahamu hivi: “Na katika uzao wako [“mbegu yako,” NW] mataifa yote ya dunia watajibarikia.” (Mwanzo 22:18) Hilo laongezea ahadi iliyotolewa wakati wa Adamu kuhusu “mbegu” ijayo. (Mwanzo 3:15) Ndiyo, yale ambayo Yehova alimwambia Abrahamu yalithibitisha tumaini la kwamba mtu fulani—Mbegu—angekuja baadaye na kuwaletea watu wote baraka. Utapata kwamba hicho ndicho kichwa kikuu kinachopatikana kotekote katika Biblia, kikikazia kwamba kitabu hiki si mkusanyo tu wa maandishi tofauti-tofauti ya wanadamu. Na kujua kichwa kikuu cha Biblia kutakusaidia kutambua kwamba Mungu alitumia taifa moja la kale—kwa lengo la kubariki mataifa yote.—Zaburi 147:19, 20.
Jambo la kwamba Yehova alikuwa na lengo hilo katika kushughulika na Israeli laonyesha kwamba ‘yeye si mwenye ubaguzi.’ (Matendo 10:34; Wagalatia 3:14) Isitoshe, hata Mungu alipokuwa akishughulika hasa na wazao wa Abrahamu, watu wa mataifa mengine walikubaliwa kuja na kumtumikia Yehova pia. (1 Wafalme 8:41-43) Na, kama tutakavyoona baadaye, kutobagua kwa Mungu ni kwa namna ya kwamba sisi sote leo—hata tuwe wa kabila gani au taifa gani—tunaweza kumjua na kumpendeza.
-