-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi nikasikia sauti kubwa katika mbingu ikisema: ‘Sasa kumetukia wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu amevurumishwa chini, ambaye huwashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kumwita Shetani “mshtaki wa ndugu zetu” kunaonyesha kwamba, hata ingawa mashtaka yake dhidi ya Ayubu yalithibitishwa kuwa bandia, yeye alifuliza moja kwa moja kutilia shaka ukamilifu wa watumishi wa kidunia wa Mungu. Kwa wazi, yeye alirudia kwa pindi nyingi lile shtaka la kwamba mtu atatoa vyote alivyo navyo kwa kubadilishana na nafsi yake. Lo! jinsi Shetani ameshindwa kwa kusikitisha!—Ayubu 1:9-11; 2:4, 5.
20. Wakristo waaminifu wamemshindaje Shetani?
20 Wakristo wapakwa-mafuta, wanaohesabiwa kuwa waadilifu “kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo,” wanaendelea kutoa ushuhuda kwa Mungu na kwa Yesu Kristo ijapokuwa minyanyaso. Kwa zaidi ya miaka 120, hii jamii ya Yohana imekuwa ikielekeza kwenye lile suala kubwa linalohusiana na kukoma kwa majira ya Mataifa katika 1914. (Luka 21:24) Na sasa umati mkubwa unatumikia kishikamanifu kando yao.
-