-
Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya PetroMnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
KARIBU miaka 30 baada ya Pentekoste ya 33 W.K., mwanafunzi Yakobo—ndugu wa kambo wa Yesu—anaandika barua kwa “makabila kumi na mawili” ya Israeli la kiroho. (Yak. 1:1) Kusudi lake: kuwahimiza wawe wenye nguvu katika imani na kuvumilia majaribu. Pia, anatoa mashauri ili kurekebisha hali zenye kusumbua ambazo zimesitawi katika makutaniko.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya PetroMnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
MUNGU ANAWAPA HEKIMA WALE ‘WANAOMWOMBA KWA IMANI’
Yakobo anaandika: “Mwenye furaha ni mtu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.” Yehova anawapa hekima wale ‘wanaoendelea kuomba kwa imani’ ili wavumilie majaribu.—Yak. 1:5-8, 12.
Pia, wale ambao ni “walimu” katika kutaniko wanahitaji imani na hekima. Baada ya kusema kwamba ulimi ni “kiungo kidogo” ambacho kinaweza ‘kuutia doa mwili wote,’ Yakobo anaonya kuhusu mielekeo ya kilimwengu ambayo inaweza kuharibu uhusiano wa mtu pamoja na Mungu. Pia, anataja hatua ambazo mtu aliye mgonjwa kiroho anapaswa kuchukua ili apone.—Yak. 3:1, 5, 6; 5:14, 15.
Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:
2:13—Ni katika maana gani “rehema hufurahi kwa njia ya ushindi juu ya hukumu”? Mungu anapotutoza hesabu, anafikiria pia rehema ambayo tumewaonyesha wengine naye anatusamehe kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Mwana wake. (Rom. 14:12) Hiyo ni sababu moja inayopaswa kutuchochea kufanya rehema kuwa sifa kuu katika maisha yetu.
4:5—Ni andiko gani ambalo Yakobo ananukuu hapa? Yakobo hanukuu andiko lolote. Hata hivyo, inawezekana kwamba maneno hayo yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanategemea mawazo ya ujumla ya maandiko kama Mwanzo 6:5; 8:21; Methali 21:10; na Wagalatia 5:17.
5:20—“Yeye anayemrudisha mtenda-dhambi kutoka kwenye kosa la njia yake” ataiokoa nafsi ya nani kutoka kwenye kifo? Mkristo anayemrudisha mkosaji kutoka kwenye njia ya dhambi anaiokoa nafsi ya mtu huyo anayetubu kutokana na kifo cha kiroho na pengine kutokana na uharibifu wa milele. Mtu anayemsaidia mtenda-dhambi katika njia hiyo “atafunika dhambi nyingi” za mtenda-dhambi huyo.
Mambo Tunayojifunza:
1:14, 15. Dhambi inatokana na tamaa zisizofaa. Kwa hiyo, hatupaswi kusitawisha tamaa mbaya kwa kuendelea kuzifikiria. Badala yake, tunahitaji ‘kuendelea kufikiria’ mambo yenye kujenga na kuyajaza katika akili na mioyo yetu.—Flp. 4:8.
2:8, 9. “Kuonyesha upendeleo” ni kinyume cha “sheria ya kifalme” ya upendo. Hivyo, Wakristo wa kweli hawaonyeshi upendeleo.
2:14-26. ‘Tunaokolewa kupitia imani,’ na “si kutokana na matendo” ya Sheria ya Musa au yale tunayotenda tukiwa Wakristo. Hatupaswi tu kudai kwamba tuna imani. (Efe. 2:8, 9; Yoh. 3:16) Imani inapaswa kutuchochea kuwa na matendo ya kimungu.
3:13-17. “Hekima inayotoka juu” bila shaka ni bora zaidi kuliko hekima ya “kidunia, ya kinyama, ya roho waovu”! Tunapaswa ‘kuendelea kuitafuta hekima ya kimungu kama hazina zilizofichika.’—Met. 2:1-5.
3:18. Mbegu ya habari njema ya Ufalme inapaswa ‘kupandwa kwa amani na wale wanaofanya amani.’ Ni jambo la maana sana kwetu kuwa watu wanaofanya amani na si wenye majivuno, wagomvi, au watu wa fujo.
-