-
Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Mapema mwaka wa 1949, mwanamume mmoja mrefu mwenye urafiki aliitembelea familia ya Koda. Aliitwa Donald Haslett, naye alikuwa amekuja Kobe kutoka Tokyo ili kutafutia mishonari nyumba. Yeye alikuwa mishonari wa kwanza kabisa wa Mashahidi wa Yehova kuja Japani. Alipata nyumba, na mnamo Novemba 1949, mishonari kadhaa wakaja Kobe. Siku moja, mishonari watano walikuja kuitembelea familia ya Koda. Wawili kati yao, Lloyd Barry na Percy Iszlaub, walitumia muda wa dakika kumi hivi kila mmoja wakizungumza kwa Kiingereza na wale waliokuwa katika nyumba hiyo. Mishonari hao walimwita Maud dada Mkristo na yaonekana alitiwa moyo na ushirika huo. Wakati huo ndipo nilipochochewa kujifunza Kiingereza.
Mishonari hao wenye bidii walinisaidia, na hatua kwa hatua nikaelewa kweli za msingi za Biblia. Nilipata majibu kwa maswali niliyokuwa nayo tangu utotoni. Naam, Biblia inatoa tumaini la kuishi milele katika paradiso duniani na ahadi ya kufufuliwa kwa “wote wale waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho.” (Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:1, 4) Nilimshukuru Yehova kwa kufanya iwezekane kuwa na tumaini hilo kupitia dhabihu ya fidia ya Mwana wake Yesu Kristo.
Utendaji wa Kiroho Wenye Kufurahisha
Kuanzia Desemba 30, 1949, mpaka Januari 1, 1950, kusanyiko la kwanza nchini Japani lilifanywa kwenye makao ya mishonari ya Kobe. Nilienda huko pamoja na Maud. Ukiwa kwenye nyumba hiyo kubwa iliyokuwa ya askari mmoja wa Nazi, ungeweza kuona vizuri Kisiwa cha Awaji na Bahari Iliyo Katikati ya Visiwa. Kwa kuwa sikuifahamu sana Biblia, nilielewa mambo machache sana yaliyosemwa. Hata hivyo, nilivutiwa sana na mishonari waliochangamana kwa uhuru na Wajapani. Watu 101 walihudhuria hotuba ya watu wote kwenye kusanyiko hilo.
Muda mfupi baada ya hapo, niliamua kushiriki katika mahubiri. Nilihitaji ujasiri ili kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa kuwa nilikuwa mwenye haya. Asubuhi moja, Ndugu Lloyd Barry alikuja nyumbani kwetu kunichukua ili twende kuhubiri pamoja. Alianza kuhubiri nyumba iliyokuwa karibu na ya Dada Koda. Nilikuwa karibu nimejificha kabisa nyuma yake huku nikisikiliza alipokuwa akihubiri. Mara ya pili nilienda kuhubiri na mishonari wengine wawili. Mwanamke mmoja Mjapani aliyekuwa mzee alitukaribisha na kutusikiliza, na baadaye akatupatia kila mmoja wetu glasi ya maziwa. Alikubali funzo la Biblia la nyumbani na mwishowe akabatizwa na kuwa Mkristo. Ilitia moyo kuona maendeleo aliyofanya.
-
-
Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Navutiwa na Undugu wa Ulimwenguni Pote
Baada ya muda mfupi, nilishangaa kupokea mwaliko wa kuhudhuria darasa la 22 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower. Mimi na Ndugu Tsutomu Fukase tulikuwa Wajapani wa kwanza kualikwa katika shule hiyo. Katika mwaka wa 1953, kabla ya darasa kuanza, tuliweza kuhudhuria Kusanyiko la Jamii ya Ulimwengu Mpya katika Uwanja wa Yankee huko New York. Nilivutiwa sana na undugu wa ulimwenguni pote wa watu wa Yehova.
Siku ya tano ya kusanyiko hilo, wajumbe kutoka Japani, hasa mishonari, walipaswa kuvaa kimono. Kwa kuwa kimono nilichokuwa nimetuma mapema hakikuwa kimefika, niliazima kimoja kutoka kwa Dada Knorr. Kusanyiko lilipokuwa likiendelea kulianza kunyesha, na nikawa na wasiwasi kwamba kimono kingelowa maji. Wakati huo, mtu fulani alinifunika kwa koti la mvua kutoka nyuma. Dada mmoja aliyekuwa amesimama kando yangu aliniuliza, “Je, unajua mtu huyo ni nani?” Baadaye niliambiwa kwamba alikuwa Ndugu Frederick W. Franz, mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Nilihisi jinsi tengenezo la Yehova lilivyo na upendo!
Darasa la 22 la Gileadi lilikuwa la kimataifa kwelikweli kwa kuwa lilikuwa na wanafunzi 120 kutoka nchi 37. Ingawa nyakati nyingine haikuwa rahisi kuwasiliana kwa sababu tulizungumza lugha mbalimbali, tulifurahia kikamili undugu wa ulimwenguni pote. Siku moja yenye theluji mnamo Februari 1954, nilihitimu na kupokea mgawo wa kurudi Japani. Mwanadarasa mwenzangu, Inger Brandt, dada kutoka Sweden, ndiye angekuwa mwenzi wangu huko Nagoya City. Huko, tulijiunga na kikundi cha mishonari waliokuwa wamehamishwa kutoka Korea kwa sababu ya vita. Nilithamini sana miaka michache niliyotumikia nikiwa mishonari.
-
-
Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Wale ndugu wanne mishonari na yule dada aliyetutembelea nyumbani kwa Dada Koda mwaka wa 1949, na vilevile Dada Maud Koda, wote walikufa wakiwa waaminifu.
-
-
Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Ninapofikiria wakati uliopita, ninahisi kwamba badiliko muhimu lilitokea maishani mwangu nilipokutana na Maud mwaka wa 1941. Kama singalikutana naye wakati huo na kama singalikubali ombi lake kumfanyia kazi tena baada ya vita, labda ningaliendelea kuishi kwenye shamba letu katika kijiji cha mbali na singalikutana na mishonari siku hizo za mapema. Ninamshukuru sana Yehova kwa kunivuta niijue kweli kupitia Maud na mishonari waliokuwa wa kwanza kuja Japani.
-
-
Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 27]
Nikiwa pamoja na mishonari kutoka Japani kwenye Uwanja wa Yankee mwaka wa 1953. Mimi niko kushoto kabisa
-