Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
    • Kufurahia Utumishi Tukiwa Wenzi wa Ndoa

      Mnamo Septemba 1957, nilialikwa kutumikia kwenye Betheli ya Tokyo. Ofisi ya tawi ya Japani ilikuwa nyumba ya mbao ya orofa mbili. Tulikuwa wanne tu katika ofisi hiyo ya tawi, kutia ndani Ndugu Barry, aliyekuwa mwangalizi wa tawi. Washiriki wale wengine wa Betheli walikuwa mishonari. Nilipewa mgawo wa kutafsiri na kusahihisha tafsiri, na pia kazi ya usafi, kufua nguo, kupika na kadhalika.

      Kazi nchini Japani ilikuwa inapanuka, na ndugu zaidi walialikwa Betheli. Mmoja wao alikuwa mzee katika kutaniko langu. Katika mwaka wa 1966, mimi na ndugu huyo anayeitwa Junji Koshino, tulioana. Baada ya kuoana, Junji alipewa mgawo wa kuwa mwangalizi wa mzunguko. Tulifurahi kuwajua ndugu na dada wengi sana tulipotembelea makutaniko mbalimbali. Kwa kuwa nilikuwa nimepewa kazi ya kutafsiri, niliifanyia mahali tulipokuwa tukikaa kila juma. Tulipokuwa tukisafiri, ilitubidi kubeba kamusi nzito pamoja na sanduku letu na mifuko mingine.

      Tulifurahia kazi ya kutembelea makutaniko kwa zaidi ya miaka minne na kuona tengenezo likizidi kukua. Ofisi ya tawi ilihamishiwa Numazu, na miaka kadhaa baadaye ikahamishiwa Ebina, mahali ilipo leo. Mimi na Junji tumefurahia utumishi wa Betheli kwa muda mrefu, na sasa tunafanya kazi pamoja na Wanabetheli wapatao 600.

  • Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
    • [Picha katika ukurasa wa 28]

      Nikiwa Betheli pamoja na mume wangu, Junji

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki