-
‘Mambo Aliyotenda Yanaambatana Naye Moja kwa Moja’Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
‘Mambo Aliyotenda Yanaambatana Naye Moja kwa Moja’
THEODORE JARACZ, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, alikufa Jumatano (Siku ya tatu) asubuhi, Juni 9, 2010 (9/6/2010) akiwa na tumaini la kwenda mbinguni. Alikuwa na umri wa miaka 84 na ameacha mke wake Melita, ambaye ameishi naye kwa miaka 53. Ameacha watu wengine kutia ndani dada yake mmoja, mpwa mmoja wa kiume, na pia wapwa wawili wa kike.
-
-
‘Mambo Aliyotenda Yanaambatana Naye Moja kwa Moja’Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Ingawa tunahuzunika sana kwa sababu ya kifo cha mfanyakazi huyo mwenye bidii na mshiriki mpendwa wa familia ya Betheli na ya undugu wa ulimwenguni pote, tunashangilia kwa sababu Ndugu Jaracz amemtumikia Yehova kwa ushikamanifu kwa miaka mingi. Tuna hakika kwamba ‘amekuwa mwaminifu hata kufikia kifo na amepokea taji la uzima.’ (Ufu. 2:10) Pia, tuna hakika kwamba ‘mambo aliyotenda yanaambatana naye moja kwa moja.’—Ufu. 14:13.
-