Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kaa Salama Ukiwa Sehemu ya Tengenezo la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 1
    • Tengenezo la Yehova

      3, 4. (a) Kulingana na kamusi moja na vilevile Mnara wa Mlinzi, tengenezo ni nini? (b) Ushirika wa kimataifa wa Mashahidi wa Yehova waweza kuitwa tengenezo katika maana gani?

      3 Kulingana na kamusi ya Oxford Dictionary, tengenezo ni “kikundi cha watu waliopangwa kitengenezo.” Kwa kukumbuka hilo twaelewa kwamba, kwa sababu mitume waliwapanga kitengenezo Wakristo wa karne ya kwanza ili kufanyiza makutaniko ya mahali walipoishi yakiwa chini ya usimamizi wa baraza linaloongoza lililokuwa Yerusalemu, inafaa kuutaja ‘ushirika huo wa ndugu’ kuwa tengenezo. (1 Petro 2:17) Leo Mashahidi wa Yehova wana muundo wa kitengenezo sawa na huo. Muungano wa ushirika huo wa karne ya kwanza uliimarishwa na “zawadi zikiwa wanadamu,” kama vile “wachungaji na walimu.” Baadhi yao walisafiri kutoka kutaniko hadi kutaniko, ilhali wengine walikuwa wazee katika makutaniko ya mahali walipoishi. (Waefeso 4:8, 11, 12; Matendo 20:28) “Zawadi” sawa na hizo huimarisha Mashahidi wa Yehova leo.

      4 Toleo la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 1922, (la Kiingereza), lilisema hivi kuhusu neno “tengenezo”: “Tengenezo ni ushirika wa watu kwa kusudi la kutimiza mpango fulani.” Gazeti la Mnara wa Mlinzi liliendelea kueleza kwamba kuwaita Mashahidi wa Yehova tengenezo hakukuwafanya wawe “madhehebu katika maana ambayo neno hilo hutumiwa, lakini tengenezo humaanisha tu kwamba Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] wanajitahidi sana kutimiza makusudi ya Mungu, wakifanya hivyo kwa njia ya utaratibu kama vile Bwana afanyavyo kila jambo.” (1 Wakorintho 14:33) Mtume Paulo alionyesha kwamba Wakristo walioishi siku yake hali kadhalika walitenda kwa njia ya utaratibu. Aliulinganisha ushirika wa Wakristo watiwa-mafuta na mwili wa binadamu, ambao una viungo vingi, kila kimoja kikitimiza fungu kilichogawiwa ili mwili uweze kufanya kazi ifaavyo. (1 Wakorintho 12:12-26) Hicho ni kielezi bora kabisa cha tengenezo! Kwa nini Wakristo walipangwa kitengenezo? Ili kutimiza “makusudi ya Mungu,” kufanya mapenzi ya Yehova.

      5. Tengenezo la Mungu lenye kuonekana ni nini?

      5 Biblia ilitabiri kwamba Wakristo wa kweli leo wangekuwa wenye muungano, wakiletwa pamoja katika “nchi” moja wakiwa “taifa,” ambamo ‘wangeng’aa wakiwa wamulikaji katika ulimwengu.’ (Isaya 66:8; Wafilipi 2:15) “Taifa” hilo lililopangwa kitengenezo sasa lina idadi ya watu zaidi ya milioni tano na nusu. (Isaya 60:8-10, 22) Hata hivyo, tengenezo la Mungu ni kubwa zaidi. Malaika pia wanatiwa ndani.

      6. Katika maana iliyo pana zaidi, ni nani wafanyizao tengenezo la Mungu?

      6 Kuna visa vingi ambapo malaika wamefanya kazi pamoja na watumishi wa kibinadamu wa Mungu. (Mwanzo 28:12; Danieli 10:12-14; 12:1; Waebrania 1:13, 14; Ufunuo 14:14-16) Kwa kufaa basi, toleo la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 1925, (la Kiingereza), lilisema: “Malaika watakatifu wote ni sehemu ya tengenezo la Mungu.” Kwa kuongezea lilisema: “Kichwa cha tengenezo la Mungu [ni] Bwana Yesu Kristo, aliye na nguvu na mamlaka yote.” (Mathayo 28:18) Kwa sababu hiyo, katika maana yake iliyo pana zaidi, tengenezo la Mungu lafanyizwa na wote walio mbinguni na duniani, ambao kwa pamoja hufanya mapenzi ya Mungu. (Ona sanduku.) Ni pendeleo lililoje kuwa sehemu ya tengenezo hilo! Na ni furaha iliyoje kutazamia kwa hamu wakati ambapo viumbe hai wote, wa kimbingu na wa kidunia, watapangwa kitengenezo kumsifu Yehova Mungu kwa muungano! (Ufunuo 5:13, 14) Lakini, ni ulinzi gani ambao tengenezo la Mungu hutoa leo?

  • Kaa Salama Ukiwa Sehemu ya Tengenezo la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 1
    • Tengenezo la Mungu ni nini?

      Katika fasihi ya Mashahidi wa Yehova, usemi “tengenezo la Mungu” hutumiwa katika njia tatu.

      1 Tengenezo la Yehova la kimbingu lisiloonekana ambalo limefanyizwa na viumbe waaminifu wa roho. Katika Biblia hilo linaitwa “Yerusalemu la juu.”—Wagalatia 4:26.

      2 Tengenezo la Yehova la kibinadamu lenye kuonekana. Leo hilo latia ndani mabaki watiwa-mafuta pamoja na umati mkubwa.

      3 Tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima. Leo, hilo latia ndani tengenezo la Yehova la kimbingu pamoja na watiwa-mafuta wake, waliofanywa kuwa wana duniani, ambao wana tumaini la kiroho. Baada ya muda, litatia ndani pia wanadamu waliofanywa wakamilifu duniani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki