Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Pendeleo la Utumishi wa Betheli

      Wengine hutumikia wakiwa washiriki wa familia ya Betheli ya duniani pote. Hao ni wafanyakazi walio wahudumu wa wakati wote ambao wamejitolea kufanya lolote watakalogawiwa kufanya katika kutayarisha na kuchapa fasihi za Biblia, katika kushughulikia kazi ya lazima ofisini, na katika kuandaa utumishi wa kutegemeza shughuli hizo. Hiyo si kazi ambayo wao hujipatia umashuhuri wa kibinafsi au mali za kimwili. Tamaa yao ni kumheshimu Yehova, na wanaridhika na upaji wanaopewa kama vile chakula, malazi, na rudishio la fedha la kiasi kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi. Kwa sababu ya aina ya maisha ya familia ya Betheli, wenye mamlaka wa kilimwengu katika Marekani, kwa kielelezo, huwaona kuwa jamii ya dhehebu la kidini ambao wamechukua nadhiri ya umaskini. Wale walio katika Betheli hupata shangwe kuweza kutumia maisha zao kikamili katika utumishi wa Yehova na katika kufanya kazi ambayo hunufaisha idadi kubwa ya ndugu zao za Kikristo na watu ambao wamependezwa karibuni, nyakati nyingine kimataifa. Kama vile wale Mashahidi wa Yehova wengineo, wao pia hushiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani.

      Familia ya kwanza ya Betheli (au familia ya Bible House, kama walivyojulikana wakati huo) ilikuwa katika Allegheny, Pennsylvania. Kufikia 1896, wafanyakazi walikuwa 12. Katika 1992, kulikuwa na washiriki wa familia ya Betheli zaidi ya 12,900, wakitumikia katika nchi 99. Kwa kuongezea, wakati nafasi ya nyumba katika majengo ya Sosaiti imekuwa haitoshi, mamia ya wafanyakazi wengine wa kujitolea wamesafiri kwenda kwenye makao ya Betheli na viwanda kila siku ili kushiriki katika kazi. Wao hulihesabu kuwa pendeleo kuwa na sehemu katika kazi inayofanywa. Kunapokuwa na uhitaji, maelfu ya Mashahidi wengineo hujitolea kuacha kazi za kimwili na utendaji mwingineo kwa vipindi vya wakati vinavyotofautiana ili kusaidia katika kujenga vifaa vinavyohitajiwa na Sosaiti vya kutumiwa kuhusiana na kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu duniani pote.

      Washiriki wengi wa familia ya Betheli ya duniani pote wameifanya iwe kazi-maisha yao. Frederick W. Franz, ambaye katika 1977 alikuja kuwa msimamizi wa nne wa Watch Tower Society, alikuwa tayari amekuwa mshiriki wa familia ya Betheli katika New York kwa miaka 57, na akaendelea katika utumishi wa Betheli kwa miaka mingine 15, mpaka alipokufa katika 1992. Heinrich Dwenger alianza utumishi wa Betheli Ujerumani katika 1911, baadaye akatumikia kwa unyenyekevu mahali popote alipogawiwa; na katika 1983, mwaka aliokufa, bado alikuwa anafurahia utumishi wake akiwa mshiriki wa familia ya Betheli katika Thun, Uswisi. George Phillips, kutoka Scotland, alikubali mgawo wa kwenda ofisi ya tawi ya Afrika Kusini katika 1924 (ilipokuwa ikisimamia utendaji wa kuhubiri toka Cape Town hadi Kenya) na akaendelea kutumikia katika Afrika Kusini hadi kifo chake katika 1982 (wakati ambapo ofisi za tawi saba za Sosaiti na Mashahidi 160,000 walikuwa watendaji katika eneo hilo). Dada Wakristo, kama vile Kathryn Bogard, Grace DeCecca, Irma Friend, Alice Berner, na pia Mary Hannan, wakiwa watu wazima walitoa maisha zao katika utumishi wa Betheli, wakifanya hivyo hadi kifo chao. Vilevile washiriki wengineo wa familia ya Betheli wamekuwa wakitumikia kwa miaka 10, 30, 50, 70, na zaidi.g

  • “Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 296, 297]

      Utumishi wa Betheli

      Kufikia 1992, kulikuwa na 12,974 waliokuwa wakishiriki katika utumishi wa Betheli katika nchi 99

      [Picha]

      Funzo la kibinafsi ni la maana kwa washiriki wa familia ya Betheli

      Hispania

      Kwenye kila Kao la Betheli, siku huanza kwa mazungumzo ya andiko la Biblia

      Finland

      Kama vile ilivyo na Mashahidi wa Yehova kila mahali, washiriki wa familia ya Betheli hushiriki katika utumishi wa shambani

      Uswisi

      Kila Jumatatu jioni familia ya Betheli hujifunza “Mnara wa Mlinzi” pamoja

      Italia

      Kazi hutofautiana, lakini yote hufanywa kwa kutegemeza kazi ya kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu

      Ufaransa

      Papua New Guinea

      Marekani

      Ujerumani

      Filipino

      Mexico

      Uingereza

      Nigeria

      Uholanzi

      Brazili

      Japani

      Afrika Kusini

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki