Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Siri Ambayo Wakristo Hawathubutu Kuweka!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 1
    • 14. Kwa nini hatupaswi kusitasita juu ya kuwa wazi katika ibada yetu?

      14 Katika mahali pengi Mashahidi wa Yehova wanazidi kupata uangalifu wa vyombo vya habari. Kama ilivyowatukia Wakristo wa mapema, mara nyingi wao huwakilishwa vibaya na huwekwa katika kundi moja na madhehebu ya kidini na mashirika ya siri yenye kutilika shaka. (Matendo 28:22) Je, huenda uwazi wetu katika kuhubiri ukatufanya tuelekee zaidi kushambuliwa? Bila shaka lingekuwa jambo lisilo la hekima, na lisilopatana na shauri la Yesu, kujitia kimbelembele katikati ya ubishi isivyo lazima. (Mithali 26:17; Mathayo 10:16) Hata hivyo, kazi yenye kunufaisha ya kuhubiri Ufalme na kusaidia watu waboreshe maisha yao haipasi kufichwa. Yamtukuza Yehova, ikimkweza, ikielekeza uangalifu kwake na kwa Ufalme wake uliosimamishwa. Itikio la juzijuzi lenye kupendeza la kweli ya Biblia katika Ulaya Mashariki na sehemu za Afrika kwa sehemu limekuwa kwa sababu ya uwazi ulioongezeka ambao sasa kweli yaweza kuhubiriwa kwao.

      15, 16. (a) Uwazi wetu na ufanisi wetu wa kiroho hutimiza kusudi gani, lakini je, hilo lituhangaishe? (b) Kwa nini Yehova huweka kulabu katika mataya ya Shetani?

      15 Ni kweli kwamba uwazi ambao Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema kwao, paradiso ya kiroho wanayofurahia, na ufanisi wao—katika nguvu za kibinadamu na pia mali za kimwili—waonekana. Huku yakiwavuta wenye moyo wa haki, mambo hayo yaweza kuwafukuza wapinzani. (2 Wakorintho 2:14-17) Kwa hakika, huenda hatimaye ufanisi huo ukatumika kushawishi majeshi ya Shetani yashambulie watu wa Mungu.

  • Siri Ambayo Wakristo Hawathubutu Kuweka!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 1
    • 18. (a) Watu wengi leo wanakuja kung’amua nini, na kwa nini? (b) Itikio la kuhubiriwa kwa Ufalme latumikaje likiwa kichocheo chenye nguvu?

      18 Katika nyakati za kisasa Mashahidi wa Yehova wamekuwa wazi sana katika kueleza maoni yao yenye kutegemea Biblia, ingawa hilo halijawa maarufu. Kwa miongo kadhaa wameonya juu ya hatari za kuvuta sigareti na matumizi mabaya ya dawa, mazoezi ya mtoto yenye uendekevu bila kufikiria mambo ya wakati ujao, matokeo mabaya ya vitumbuizo vilivyojawa na ngono haramu na jeuri, na hatari za kutiwa damu mishipani. Pia wameonyesha kutopatana mbalimbali kwa nadharia ya mageuzi. Watu zaidi na zaidi sasa wanasema, “Mashahidi wa Yehova hawajakosea hata hivyo.” Tusingalikuwa wazi hivyo katika kujulisha maoni yetu hadharani, hawangeitikia hivyo. Na usipuuze lile jambo la hakika la kwamba kwa kutoa taarifa hiyo, wanachukua hatua kuelekea kusema, “Shetani, wewe ni mwongo; hata hivyo, Yehova ni wa kweli.” Twachochewa kwa nguvu kama nini tuendelee kufuata kielelezo cha Yesu, kusema hadharani neno la kweli!—Mithali 27:11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki