-
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya KwanzaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Sura ya 3
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya Kwanza
“MTAKUWA mashahidi wangu . . . hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Mdo. 1:8, NW) Kwa maneno hayo ya kuaga, Yesu aliwapa wanafunzi wake utume wa kuwa mashahidi. Lakini mashahidi wa nani? “Mashahidi wangu,” akasema Yesu. Je, maneno hayo yamaanisha kwamba hawakupaswa kuwa mashahidi wa Yehova? Hata!
Kwa kweli, wanafunzi wa Yesu walipewa pendeleo lisilo na kifani—lile la kuwa mashahidi wa wote wawili, Yehova na Yesu. Wakiwa Wayahudi waaminifu, wanafunzi wa mapema wa Yesu walikuwa tayari ni mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Lakini sasa walipaswa kutoa ushahidi pia kwa habari ya fungu muhimu la Yesu katika kutakaswa kwa jina la Yehova kupitia Ufalme Wake wa Kimesiya. Kutoa ushahidi hivyo juu ya Yesu, kulimtukuza Yehova. (Rum. 16:25-27; Flp. 2:9-11) Walishuhudia kwamba Yehova hakuwa amesema uwongo, kwamba baada ya miaka zaidi ya 4,000 alikuwa hatimaye amemwinua Mesiya, au Kristo, aliyekuwa ameahidiwa kwa muda mrefu!
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova katika karne ya kwanza walipewa pia daraka lisilo na kifani—daraka ambalo ni la Wakristo wa kweli mpaka leo hii.
“Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
Baada ya ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu, aliwatokea wanafunzi wake waliokuwa wamekusanyika kwenye mlima mmoja katika Galilaya. Huko, Yesu alieleza daraka lao: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo mimi nimewaamuru nyinyi. Na, tazameni! mimi nipo pamoja nanyi siku zote hadi umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt. 28:19, 20, NW)
-
-
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya KwanzaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hivyo utume mzito ulipewa wafuasi wa Kristo, yaani, kutenda kazi ya kufanya wanafunzi miongoni mwa mataifa yote. Ingawa hivyo, ili wafanye wanafunzi wa Kristo ilikuwa lazima watoe ushahidi kwa habari ya jina na Ufalme wa Yehova, kwa maana hivyo ndivyo Kielelezo chao, Yesu, alivyokuwa ametenda. (Luka 4:43; Yn. 17:26) Hivyo, wale waliokubali fundisho la Kristo na kuwa wanafunzi walikuja kuwa mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Kuwa shahidi wa Yehova hakukuwa tena jambo la kuzaliwa—ndani ya taifa la Kiyahudi—bali la kujichagulia. Wale waliokuja kuwa mashahidi walifanya hivyo kwa sababu walimpenda Yehova na walitaka kwa moyo mweupe kujitiisha kwa utawala wake wa enzi kuu.—1 Yoh. 5:3.
-