Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Uthamini Wenye Kukua Kuelekea Jina la Mungu

      Hatua kwa hatua hao Wanafunzi wa Biblia walizidi kufahamu umaarufu ambao Maandiko yaliyopuliziwa yalilipa jina la kibinafsi la Mungu. Jina hilo lilikuwa limefichwa katika Kiingereza na tafsiri za Biblia za Douay ya Roma Katoliki na King James ya Protestanti, kama vile baadaye ilivyofanywa na tafsiri kadhaa katika lugha nyingi katika karne ya 20. Lakini tafsiri mbalimbali pamoja na vitabu vya marejezo kwenye Biblia vilishuhudia kwamba jina Yehova lapatikana mara elfu nyingi katika maandishi ya lugha za awali—kwa kweli mara nyingi zaidi ya jina jingine lolote, na mara nyingi zaidi ya jumla iliyounganishwa ya majina ya cheo kama vile Mungu na Bwana. Wakiwa “watu kwa ajili ya jina lake,” uthamini wao wenyewe kuelekea jina hilo la kimungu ulikua. (Mdo. 15:14, NW) Katika The Watch Tower la Januari 1, 1926, walitoa lile walilotambua kuwa suala ambalo lazima kila mtu alikabili, yaani, “Ni Nani Atamheshimu Yehova?”

      Mkazo ambao waliweka juu ya jina la Mungu haukuwa jambo la ujuzi tu wa kidini. Kama ilivyoelezwa katika kitabu Prophecy (kilichotangazwa 1929), suala kuu linalokabili uumbaji wote wenye akili lahusu jina na neno la Yehova Mungu. Mashahidi wa Yehova hukazia kwamba Biblia huonyesha kwamba lazima kila mtu ajue jina la Mungu na kulitendea kuwa takatifu. (Mt. 6:9; Eze. 39:7) Lazima liondolewe suto lote ambalo limerundikiwa, si na wale tu ambao wamekuwa wakaidi waziwazi kwa Yehova bali pia na wale ambao wamemwakilisha vibaya kwa mafundisho na matendo yao. (Eze. 38:23; Rum. 2:24) Kwa msingi wa Maandiko, Mashahidi hutambua kwamba hali njema ya ulimwengu wote mzima na wakaaji wao yategemea kutakaswa kwa jina la Yehova.

      Wajua kwamba kabla Yehova hajachukua hatua ya kuwaharibu waovu, ni wajibu na pendeleo la mashahidi wake kuwaambia wengine kweli juu yake. Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakifanya hivyo duniani kote. Wamekuwa wenye bidii sana katika kutimiza daraka hilo hivi kwamba, kimataifa, yeyote ambaye hutumia sana jina Yehova anatambuliwa haraka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 124]

      Kujulisha Jina la Mungu

      ◆ Tangu 1931 jina Mashahidi wa Yehova limetumiwa kuonyesha wale ambao huabudu na kumtumikia Yehova akiwa Mungu pekee wa kweli.

      ◆ Tangu Oktoba 15, 1931, jina la Mungu la kibinafsi, Yehova, limeonekana juu ya jalada la mbele la kila toleo la gazeti “Mnara wa Mlinzi.”

      ◆ Katika wakati ambao jina la Mungu la kibinafsi lilikuwa likiacha kutiwa katika tafsiri nyingi za kisasa za Biblia, Mashahidi wa Yehova walianza kutangaza, katika 1950, “New World Translation,” ambayo ilirudisha jina la Mungu kwenye mahali palipo haki yalo.

      ◆ Kuongezea Biblia yenyewe, fasihi nyingine nyingi zimetangazwa na Watch Tower Bible and Tract Society ili kukaza uangalifu wa pekee kwenye jina la Mungu—kwa kielelezo, vitabu “Jehovah” (1934), “Let Your Name Be Sanctified” (1961), na “‘The Nations Shall Know That I Am Jehovah’—How?” (1971), pamoja na broshua “Jina la Mungu Litakaloendelea Milele” (1984).

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki