Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Katika mahali pamoja baada ya pengine, Mashahidi wa Yehova wamelazimika kukabili hali zilizotatiza kutokuwamo kwao kwa Kikristo. Serikali zilizokuwa zikitawala katika Amerika ya Latin, Afrika, Mashariki ya Kati, Ireland Kaskazini, na kwingineko zimekabili upinzani wa jeuri kutoka kwa majeshi ya kimapinduzi. Likiwa tokeo, serikali na majeshi ya upinzani pia yamesonga Mashahidi wa Yehova waunge mkono kwa tendo. Lakini Mashahidi wa Yehova wamedumisha kutokuwamo kamili. Baadhi yao wamepigwa kikatili, hata kuuawa, kwa sababu ya msimamo waliochukua. Hata hivyo, mara nyingi, kutokuwamo halisi kwa Kikristo kwa Mashahidi wa Yehova kumewapatia staha kutoka kwa maofisa wa pande zote mbili, nao Mashahidi huruhusiwa kuendelea bila kusumbuliwa katika kazi yao ya kuwaambia wengine habari njema juu ya Ufalme wa Yehova.

      Katika miaka ya 1960 na ya 1970, kutokuwamo kwa Mashahidi kulipatwa na mitihani ya kinyama kuhusiana na dai la kwamba raia wote wa Malawi wanunue kadi iliyoonyesha uanachama katika chama cha kisiasa chenye kutawala. Mashahidi wa Yehova waliliona jambo hilo kuwa kinyume cha imani zao za Kikristo kushiriki katika hilo. Likiwa tokeo, walipatwa na mnyanyaso usio na kifani katika ukatili wake wenye kuumiza. Makumi ya maelfu walilazimika kutoroka nchi hiyo, na baada ya wakati wengi walirudishwa nchini kwa nguvu wakakabili unyama zaidi.

  • “Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 195]

      Si Tisho kwa Serikali Yoyote

      ◆ Ilipokuwa ikiandika juu ya walivyotendewa Mashahidi wa Yehova katika nchi moja ya Amerika ya Latini, tahariri moja katika “World-Herald” la Omaha, Nebraska, Marekani, ilisema: “Yataka uwazio wa ushupavu wa upande mmoja na hofu isiyo na msingi kuamini kwamba Mashahidi wa Yehova hutokeza tisho la aina yoyote kwa serikali yoyote ya kisiasa; wao si wataka-mapinduzi na ni wapenda amani wakiwa kikundi cha kidini kadiri iwezekanavyo, nao huomba tu kwamba waruhusiwe kufuatia imani yao kwa njia yao wenyewe.”

      ◆ “Il Corriere di Trieste,” gazeti moja la habari la Italia, lilitaarifu hivi: “Mashahidi wa Yehova wapasa kusifiwa kwa ajili ya imara na ushikamano wao. Tofauti na dini nyinginezo, umoja wao wakiwa kikundi cha watu huwazuia kutosali kwa Mungu yuleyule mmoja, katika jina la Kristo yuleyule mmoja, abariki pande mbili zenye kupingana katika pigano, au kutochanganya siasa na dini ili kutumikia masilahi ya Kiongozi wa Serikali au vyama vya kisiasa. La mwisho lakini lenye umaana uleule, wako tayari kukabili kifo kuliko kuvunja . . . ile amri USIUE!”

      ◆ Baada ya Mashahidi wa Yehova kuwa wamevumilia marufuku ya miaka 40 katika Chekoslovakia, gazeti la habari “Nová Svoboda” lilisema hivi, katika 1990: “Imani ya Mashahidi wa Yehova huwakataza kutumia silaha dhidi ya wanadamu, na wale waliokataa utumishi wa msingi wa kijeshi na hawakufanya kazi katika migodi ya makaa-mawe walikwenda gerezani, hata kwa miaka minne. Kutokana na hilo tu ni wazi kwamba wana imara kubwa ya kiadili. Tungeweza kutumia watu kama hao wasio na ubinafsi hata katika shughuli za kisiasa za juu kabisa—lakini hatutaweza kamwe kuwaingiza humo. . . . Bila shaka, watambua mamlaka za kiserikali lakini waamini kwamba ni Ufalme wa Mungu tu uwezao kutatua matatizo yote ya kibinadamu. Lakini usikosee—wao hawashikilii mambo bila kutumia akili. Ni watu ambao hujishughulisha sana na wanadamu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki