Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Wenye Kuendelea, Si Wenye Kufungwa na Itikadi za Kidini

      Uelewevu wa wazi wa Neno la Mungu haukuja mara hiyo. Katika visa vingi Wanafunzi wa Biblia walifahamu jambo moja katika kile kigezo cha kweli lakini hawakuelewa kila jambo. Hata hivyo, wao walikuwa tayari kujifunza. Hawakufungwa na itikadi za kidini; walikuwa wenye kuendelea. Yale waliyojifunza walishiriki na wengine. Wao hawakujisifu kwa mambo waliyofundisha; walitafuta ‘kufundishwa na Yehova.’ (Yn. 6:45, NW) Nao walikuja kuthamini kwamba Yehova huwezesha kuwa na uelewevu wa mambo madogomadogo ya kusudi lake katika wakati wake mwenyewe na katika njia yake mwenyewe.—Dan. 12:9; linganisha Yohana 16:12, 13.

      Kujifunza mambo mapya hutaka marekebisho katika maoni. Ikiwa makosa yatakubaliwa na mabadiliko yenye manufaa kufanywa, unyenyekevu wahitajiwa. Sifa hiyo na matunda yayo yatamanika kwa Yehova, na mwendo kama huo huvuta sana wapendao kweli. (Sef. 3:12) Lakini unadhihakiwa na wale ambao hujisifia itikadi za kidini ambazo zimeendelea bila kubadilika kwa karne nyingi, ingawa hizo zilifanyizwa na wanadamu wasiokamilika.

  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 133]

      Kweli Yenye Kuendelea

      Katika 1882, C. T. Russell aliandika hivi: “Biblia ndiyo kiwango chetu pekee, na mafundisho yayo ni itikadi yetu pekee ya kidini, na kwa kutambua hali yenye kuendelea ya kufunguka kwa kweli za Kimaandiko, sisi tuko tayari na tumejitayarisha kuongeza au kurekebisha itikadi yetu ya kidini (imani) kadiri tupatavyo ongezeko la nuru kutoka katika Kiwango chetu.” —“Watch Tower,” Aprili 1882, uku. 7.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki