Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Tulivyokuja Kujulikana Kuwa Mashahidi wa Yehova
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mitume wa Kristo walipokuwa wangali hai, jina Wakristo lilikuwa lenye kutofautisha na mahususi. (1 Pet. 4:16) Wote waliodai kuwa Wakristo lakini ambao imani zao au mwenendo vilipinga dai lao walifukuzwa kutoka jumuiya ya Kikristo. Hata hivyo, kama vile Yesu alivyokuwa ametabiri, baada ya kifo cha mitume Shetani alipanda mbegu ambazo zilitokeza Wakristo wa mwigo. Watu hao bandia walidai pia kutumia jina Wakristo. (Mt. 13:24, 25, 37-39) Ukristo wenye kuasi imani ulipotumia njia ya kugeuza watu kwa nguvu, wengine walidai kuwa Wakristo ili tu waepuke mnyanyaso. Baada ya wakati, Mzungu yeyote asiyedai kuwa Myahudi, Mwislamu, au Mwatheisti mara nyingi alionwa kuwa Mkristo, bila kujali imani au mwenendo wake.

  • Jinsi Tulivyokuja Kujulikana Kuwa Mashahidi wa Yehova
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Uhitaji wa Jina Lenye Kutofautisha

      Baada ya wakati, ikazidi kuwa wazi sana kwamba kuongezea mtajo Wakristo, kutaniko la watumishi wa Yehova kwa kweli lilihitaji jina lenye kutofautisha. Maana ya jina Wakristo ilikuwa imepotoshwa katika akili za umma kwa sababu watu waliodai kuwa Wakristo mara nyingi walikuwa na wazo kidogo tu au hawakuwa na wazo lolote juu ya Yesu Kristo alikuwa nani, yale aliyofundisha, na yale ambayo wao wapaswa kuwa wakifanya ikiwa kwa kweli walikuwa wafuasi wake. Kwa kuongezea, kadiri ndugu zetu walivyofanya maendeleo katika uelewevu wao wa Neno la Mungu, waliona waziwazi uhitaji wa kujitenga na kuwa tofauti na mifumo ya kidini iliyodai kwa udanganyifu kuwa ya Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki