Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unapaswa Kuwa Mnyoofu Nyakati Zote?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
    • Je, mtu maskini anaweza kuamini ahadi hiyo? Victorine anaamini kwamba ni ahadi ya kweli.

      Maisha ya Victorine ni magumu kwa sababu ni mjane aliye na watoto watano wanaoenda shuleni. Anaishi katika nchi inayositawi ambamo hawapati msaada wa kutosha kutoka kwa serikali. Kuna nafasi nyingi za kuiba kwa sababu wengi wanafanya kazi katika mitaa. Hata hivyo, Victorine hakubali kamwe kushawishiwa kuiba. Badala yake, anajitahidi kupata mahitaji yake kwa unyoofu kwa kuuza vitu kando ya barabara. Kwa nini anaendelea kuwa mnyoofu?

      “Kwanza, ninaamini kwamba Mungu ni mnyoofu na atanitendea kwa unyoofu ikiwa nitamwiga. Pili, watoto wangu watajifunza kuwa wanyoofu ikiwa tu wataniona nikiwa mnyoofu.”

      Matokeo yamekuwa nini? Anasema hivi: “Tuna chakula, mavazi, na makao. Hata hivyo, nyakati nyingine ninalazimika kuwaomba marafiki wanisaidie, kwa mfano, ninapohitaji pesa za kulipia matibabu ya ugonjwa wa ghafula. Sijawahi kamwe kukosa ninachohitaji. Kwa nini? Kwa sababu marafiki wangu wanajua kwamba siwadanganyi ninapowaeleza hali zangu na sijaribu kujipatia faida.

      “Watoto wangu wanajifunza kuwa wanyoofu wanapoendelea kukua. Hivi karibuni, jirani mmoja aliona sarafu chache kwenye meza yetu akaniuliza kwa nini sikuogopa kwamba watoto wangu watazichukua. Hakuamini kamwe nilipomwambia kwamba watoto wangu hawawezi kufanya hivyo. Aliamua kuwajaribu bila mimi kujua. Kwa siri aliweka sarafu mbili zenye thamani ya faranga 100 katika nyumba yetu mahali ambapo watoto wangeweza kuziona kwa urahisi. Aliporudi siku iliyofuata, alishangaa sana kuona kwamba bado sarafu hizo zilikuwapo. Kuwa na watoto wanyoofu ni jambo bora zaidi kuliko kuwa na vitu vingi vya kimwili.”

  • Je, Unapaswa Kuwa Mnyoofu Nyakati Zote?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
    • Victorine anajua kwamba matatizo yake ya kifedha yatakwisha kabisa wakati ambapo Mungu atabadili mambo. Hata hivyo, ana utajiri wa kiroho ambao hauwezi kununuliwa kwa pesa. Watoto wake ni wanyoofu na wana tabia nzuri. Kila Jumapili (Siku ya Yenga) ‘wanabubujikwa na maneno’ wanapozungumza na majirani wao kuhusu wema wa Mungu na jinsi atakavyowatosheleza “wote wanaomwitia yeye katika ukweli” na kwamba atawalinda “wale wote wanaompenda.”—Zaburi 145:7, 18, 20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki