-
Mkutano Uliokazia Umoja na Kuzungumzia Mipango Yenye KusisimuaMnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
-
-
Kuna mipango ya kujenga kwenye kiwanja cha Warwick ambacho kina ukubwa wa ekari 248. Ndugu Pierce alisema kwamba “ingawa hatujui kwa hakika mapenzi ya Yehova ni nini kuhusu Warwick, tutaanza kazi ya ujenzi ili hatimaye makao makuu ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova yahamie huko.” Mipango pia inafanywa ili kutumia kiwanja chenye ukubwa wa ekari 50 ambacho kiko umbali wa kilomita 10 upande wa kaskazini wa Warwick kwa ajili ya mashini na vifaa vya ujenzi. “Mara tu baada ya kupata kibali cha kujenga, tunatumaini kukamilisha mradi wote katika muda wa miaka minne,” akasema Ndugu Pierce. “Halafu tutauza majengo yetu ya Brooklyn.”
-
-
Mkutano Uliokazia Umoja na Kuzungumzia Mipango Yenye KusisimuaMnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 17]
Mchoro wa makao makuu ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova ambayo yanakusudiwa kujengwa huko Warwick, New York
-