Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Wapewa “Jina Jipya” na Yehova

      6. Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni?

      6 Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni, “mwanamke” wake wa kimbingu, aliyewakilishwa na Yerusalemu la kale? Anasema hivi: “Mataifa wataiona haki yako [“Ee mwanamke,” “NW”], na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.” (Isaya 62:2) Wakati Waisraeli wanapotenda uadilifu, mataifa yanalazimika kuangalia kwa makini. Hata wafalme wanalazimika kukubali kwamba Yehova anatumia Yerusalemu na kwamba utawala wowote walio nao si kitu ukilinganishwa na Ufalme wa Yehova.—Isaya 49:23.

      7. Jina jipya la Sayuni linamaanisha nini?

      7 Sasa Yehova anampa Sayuni jina jipya ili kuthibitisha kwamba hali yake imebadilika. Jina hilo jipya linamaanisha hali yenye baraka na cheo chenye heshima kinachofurahiwa na watoto wa kidunia wa Sayuni kuanzia mwaka wa 537 K.W.K.a Linaonyesha kwamba Yehova anamkubali Sayuni kuwa mali yake. Leo, Israeli wa Mungu wanasisimuka kuwa kipenzi cha Yehova kwa njia hiyo, na wale kondoo wengine wanashangilia pamoja nao.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Katika unabii wa Biblia, “jina jipya” linaweza kumaanisha cheo kipya au pendeleo jipya.—Ufunuo 2:17; 3:12.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 9. Eleza jinsi hali ya Sayuni inavyogeuzwa.

      9 Upaji wa jina jipya ni sehemu ya kumgeuza Sayuni wa kimbingu, anayewakilishwa na watoto wake wa kidunia, ili awe na hali ya kupendeza. Tunasoma hivi: “Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba [Namfurahia]; na nchi yako Beula [Ameolewa]; kwa kuwa BWANA anakufurahia, na nchi yako itaolewa.” (Isaya 62:4) Sayuni wa kidunia amekuwa ukiwa tangu alipoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. Hata hivyo, maneno ya Yehova yanamhakikishia kwamba nchi yake itarudishiwa hali yake ya kwanza na kujazwa wakaaji tena. Sayuni aliyeteketezwa wakati mmoja hatakuwa tena mwanamke aliyeachwa pweke, wala nchi yake haitakuwa ukiwa tena. Kurudishwa kwa Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. kunamaanisha kwamba atapata hali mpya, inayotofautiana kabisa na hali yake ya kwanza ya kuwa magofu. Yehova anatangaza kwamba Sayuni ataitwa “Namfurahia,” na nchi yake itaitwa “Ameolewa.”—Isaya 54:1, 5, 6; 66:8; Yeremia 23:5-8; 30:17; Wagalatia 4:27-31.

      10. (a) Hali ya Israeli wa Mungu iligeuzwaje? (b) “Nchi” ya Israeli wa Mungu ni nini?

      10 Kuanzia mwaka wa 1919 badiliko kama hilo lilipata Israeli wa Mungu. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, Wakristo watiwa-mafuta walionekana ni kama wamekataliwa na Mungu. Lakini mwaka wa 1919 walirudishiwa hali ya kukubalika, na njia yao ya kuabudu ikatakaswa. Jambo hilo liligeuza mafundisho yao, tengenezo lao, na utendaji wao. Taifa la Israeli wa Mungu liliingia katika “nchi” yake, miliki yake ya kiroho, au makao ya utendaji.—Isaya 66:7, 8, 20-22.

      11. Wayahudi wanamwoaje mama yao?

      11 Yehova anazidi kukazia hali mpya ya kukubalika kwa watu wake, anapotangaza hivi: “Kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amafurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.” (Isaya 62:5) Wayahudi, wale “wana” wa Sayuni, wanawezaje kumwoa mama yao? Katika maana ya kwamba wana wa Sayuni wanaorudi baada ya kufunguliwa watoke uhamishoni Babiloni wanamiliki jiji lao kuu la zamani na kukaa humo tena. Inapokuwa hivyo, Sayuni si mkiwa tena, bali ana wana chungu nzima.—Yeremia 3:14.

      12. (a) Yehova amejulishaje wazi kwamba Wakristo watiwa-mafuta ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika ndoa? (b) Shughuli za Yehova pamoja na watu wake zinatoaje kielelezo cha ndoa ya hali ya juu leo? (Ona sanduku katika ukurasa wa 342.)

      12 Kwa njia ya ulinganifu, tangu mwaka wa 1919 watoto wa Sayuni wa kimbingu wamemiliki nchi yao, miliki yao ya kiroho, iliyo na jina la kiunabii “Ameolewa.” Utendaji wao wa Kikristo katika nchi hiyo umeonyesha wazi kwamba Wakristo hawa watiwa-mafuta ni “watu kwa ajili ya jina lake” Yehova. (Matendo 15:14) Kuzaa kwao matunda ya Ufalme na kutangaza jina la Yehova kumeonyesha wazi kwamba Yehova huwafurahia sana Wakristo hawa. Yeye ameonyesha wazi kwamba wao ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika umoja usiovunjika. Kwa kuwatia mafuta Wakristo hawa kwa roho takatifu, kuwakomboa watoke katika utekwa wa kiroho, na kuwatumia ili wahubirie jamii yote ya wanadamu tumaini la Ufalme, Yehova ameonyesha kwamba anawashangilia kwa shangwe ya bwana-arusi kumwelekea bibi-arusi.—Yeremia 32:41.

      “Msiwe na Kimya”

      13, 14. (a) Nyakati za kale, Yerusalemu linakuwaje jiji lenye usalama? (b) Nyakati za kisasa, Sayuni amekuwaje “sifa duniani”?

      13 Jina jipya la mfano ambalo Yehova amewapa watu wake huwafanya wahisi usalama. Wanajua kwamba yeye huwakubali na kwamba wao ni miliki yake.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 339]

      Yehova atamwita Sayuni wa kimbingu kwa jina jipya

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki