Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 1
    • “Mwanamke” si Hawa bali ni tengenezo la kimbingu la Yehova, mama ya watumishi watiwa-mafuta kwa roho walio duniani. (Wagalatia 4:26)

  • Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 1
    • “Uadui Kati Yako na Huyo Mwanamke”

      6. Ni katika njia zipi Shetani ameonyesha uadui dhidi ya mwanamke wa Yehova?

      6 Katika wakati huo wote, kulikuwa na uadui kati ya Nyoka na mwanamke wa Yehova, kati ya Shetani Ibilisi na tengenezo la kimbingu la Yehova la viumbe-roho waaminifu-washikamanifu. Uadui wa Shetani ulionyeshwa alipomdhihaki Yehova na kujaribu kuvuruga tengenezo la kimbingu la Yehova, akiwashawishi malaika waache makao yao yenye kufaa. (Mithali 27:11; Yuda 6) Ulidhihirishwa wakati Shetani alipotumia roho waovu wake kujaribu kuzuia wajumbe wa kimalaika waliotumwa na Yehova. (Danieli 10:13, 14, 20, 21) Uadui huo ulionekana wazi kwa njia yenye kutokeza katika karne hii ya 20 wakati Shetani alipotaka kuharibu Ufalme wa Kimesiya wakati ulipozaliwa.—Ufunuo 12:1-4.

      7. Kwa nini malaika waaminifu-washikamanifu wa Yehova walihisi uadui dhidi ya Nyoka wa mfano, na bado wameonyesha kujizuia kupi?

      7 Uadui ulikuwako pia kwa upande wa mwanamke wa Yehova, jamii ya malaika waaminifu-washikamanifu, dhidi ya Nyoka wa ufananisho. Shetani alikuwa amechongea jina zuri la Mungu; pia alikuwa ametilia shaka uaminifu-maadili wa kila mmoja wa viumbe vya Mungu wenye akili, kutia na malaika wote, naye alikuwa akijaribu kwa bidii kukengeusha uaminifu-mshikamanifu wao kwa Mungu. (Ufunuo 12:4a) Malaika, makerubi, na maserafi waaminifu-washikamanifu, hakika wangeweza kuhisi machukio makuu dhidi ya yule aliyejifanya Ibilisi na Shetani. Hata hivyo, wamemngojea Yehova ashughulike na mambo hayo katika wakati wake na kwa njia yake mwenyewe.—Linganisha Yuda 9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki