-
Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 1
-
-
“Mwanamke” si Hawa bali ni tengenezo la kimbingu la Yehova, mama ya watumishi watiwa-mafuta kwa roho walio duniani. (Wagalatia 4:26)
-
-
Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 1
-
-
“Uadui Kati Yako na Huyo Mwanamke”
6. Ni katika njia zipi Shetani ameonyesha uadui dhidi ya mwanamke wa Yehova?
6 Katika wakati huo wote, kulikuwa na uadui kati ya Nyoka na mwanamke wa Yehova, kati ya Shetani Ibilisi na tengenezo la kimbingu la Yehova la viumbe-roho waaminifu-washikamanifu. Uadui wa Shetani ulionyeshwa alipomdhihaki Yehova na kujaribu kuvuruga tengenezo la kimbingu la Yehova, akiwashawishi malaika waache makao yao yenye kufaa. (Mithali 27:11; Yuda 6) Ulidhihirishwa wakati Shetani alipotumia roho waovu wake kujaribu kuzuia wajumbe wa kimalaika waliotumwa na Yehova. (Danieli 10:13, 14, 20, 21) Uadui huo ulionekana wazi kwa njia yenye kutokeza katika karne hii ya 20 wakati Shetani alipotaka kuharibu Ufalme wa Kimesiya wakati ulipozaliwa.—Ufunuo 12:1-4.
7. Kwa nini malaika waaminifu-washikamanifu wa Yehova walihisi uadui dhidi ya Nyoka wa mfano, na bado wameonyesha kujizuia kupi?
7 Uadui ulikuwako pia kwa upande wa mwanamke wa Yehova, jamii ya malaika waaminifu-washikamanifu, dhidi ya Nyoka wa ufananisho. Shetani alikuwa amechongea jina zuri la Mungu; pia alikuwa ametilia shaka uaminifu-maadili wa kila mmoja wa viumbe vya Mungu wenye akili, kutia na malaika wote, naye alikuwa akijaribu kwa bidii kukengeusha uaminifu-mshikamanifu wao kwa Mungu. (Ufunuo 12:4a) Malaika, makerubi, na maserafi waaminifu-washikamanifu, hakika wangeweza kuhisi machukio makuu dhidi ya yule aliyejifanya Ibilisi na Shetani. Hata hivyo, wamemngojea Yehova ashughulike na mambo hayo katika wakati wake na kwa njia yake mwenyewe.—Linganisha Yuda 9.
-