-
Kichwa Kitukufu cha BibliaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
7. Ni nini linaloonyesha kwamba mwanamke wa Mwanzo 3:15 ni wa kao la kiroho?
7 Anayefuata kusemwa na Mwanzo 3:15 ni “mwanamke.” Je! huyu alikuwa Hawa? Yawezekana Hawa alifikiri hivyo. (Linga Mwanzo 4:1.) Lakini uadui kati ya Hawa na Shetani haukuwezekana kuwa wa muda mrefu wakati Hawa alipokufa zaidi ya miaka 5,000 iliyopita. Zaidi, kwa kuwa Nyoka aliyeelekezewa maneno ya Yehova alikuwa roho asiyeonekana, imetupasa kutazamia kwamba huyo mwanamke angekuwa pia wa kao la kiroho. Ufunuo 12:1, 2 unathibitisha hilo, ukionyesha kwamba mwanamke huyu ni tengenezo la Yehova la kimbingu lenye viumbe wa roho.—Ona pia Isaya 54:1, 4, 13.
-
-
Kichwa Kitukufu cha BibliaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. Baada ya kupita karne nyingi, Mungu alifunua nini kuhusu mbegu ya mwanamke?
11 Kwa kumalizia unabii kwenye Mwanzo 3:15 unaelekeza kwa mbegu ya mwanamke. Wakati Shetani alipokuwa akisitawisha mbegu yake, Yehova alikuwa akitayarisha kwa ajili ya “mwanamke” wake, au tengenezo la kimbingu lenye mfano wa mke, litokeze mbegu.
-
-
Kichwa Kitukufu cha BibliaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
14 Katika Biblia, Wakristo wapakwa-mafuta wanaitwa ndugu za Yesu, na wakiwa nduguze, wanashiriki Baba yule yule na mama yule yule. (Waebrania 2:11) Baba yao ni Yehova Mungu. Kwa sababu hiyo, mama yao lazima awe “mwanamke,” tengenezo la Mungu la kimbingu lililo mfano wa mke.
-