-
‘Je, Moyo Wako Umenyoka Pamoja na Moyo Wangu?’Mnara wa Mlinzi—1998 | Januari 1
-
-
Yehu wa Siku ya Kisasa na Yehonadabu wa Siku ya Kisasa
5. (a) Ni mabadiliko gani ambayo karibuni yatatukia kwa wanadamu wote? (b) Ni nani aliye Yehu Mkubwa Zaidi, naye huwakilishwa na nani duniani?
5 Leo, karibuni mambo yatabadilika sana kwa wanadamu wote kama vile yalivyobadilika kwa Israeli huko nyuma mwaka wa 905 K.W.K. Wakati umekaribia ambapo Yehova ataitakasa dunia na kuondoa matokeo yote mabaya ya uvutano wa Shetani, kutia na dini isiyo ya kweli. Yehu wa siku ya kisasa ni nani? Si mwingine ila Yesu Kristo, ambaye kwake maneno haya ya unabii yaelekezwa: “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, utukufu ni wako na fahari ni yako. Katika fahari yako usitawi uendelee kwa ajili ya kweli na upole na haki.” (Zaburi 45:3, 4) Yesu awakilishwa duniani na “Israeli wa Mungu,” Wakristo watiwa-mafuta “washikao amri za Mungu na walio na kazi ya kutoa ushahidi kuhusu Yesu.” (Wagalatia 6:16; Ufunuo 12:17) Tangu mwaka wa 1922 ndugu hawa wa Yesu watiwa-mafuta wametoa onyo bila hofu juu ya matendo ya Yehova ya hukumu yanayokuja.—Isaya 61:1, 2; Ufunuo 8:7–9:21; 16:2-21.
-
-
‘Je, Moyo Wako Umenyoka Pamoja na Moyo Wangu?’Mnara wa Mlinzi—1998 | Januari 1
-
-
8. Mashahidi wa Yehova huonyeshaje bidii yao kwa ibada ya kweli?
8 Yehu alikuwa na sifa ya kuendesha gari lake kwa kasi sana—uthibitisho wa bidii yake ya kutimiza kazi yake. (2 Wafalme 9:20) Yesu, yule Yehu Mkubwa Zaidi, afafanuliwa kuwa ‘ameliwa’ na bidii. (Zaburi 69:9) Basi, haishangazi kwamba, Wakristo wa kweli leo, wajulikana kwa bidii yao. Ndani ya kutaniko na kwa watu wote, wao ‘hulihubiri neno, kwa hima katika majira yenye kufaa, katika majira yenye taabu.’ (2 Timotheo 4:2)
-