-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha YeremiaMnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
-
-
“TIENI SHINGO ZENU CHINI YA NIRA YA MFALME WA BABILONI”
Yeremia anatangaza hukumu juu ya wafalme wanne wa mwisho wa Yuda na pia juu ya manabii wa uwongo, wachungaji wabaya, na makuhani wapotovu. Akiwataja mabaki waaminifu kuwa tini nzuri, Yehova anasema hivi: “Nitaweka jicho langu juu yao kwa njia nzuri.” (Yeremia 24:5, 6) Unabii wenye sehemu tatu katika sura ya 25 unataja kwa ufupi hukumu zinazozungumziwa kwa urefu katika sura zinazofuata.
Makuhani na manabii wanapanga njama ya kumuua Yeremia. Ujumbe wake ni kwamba wanapaswa kumtumikia mfalme wa Babiloni. Yeremia alimwambia Mfalme Sedekia hivi: “Tieni shingo zenu chini ya nira ya mfalme wa Babiloni.” (Yeremia 27:12) Hata hivyo, “Yeye anayemtawanya Israeli atamkusanya [Israeli] pamoja.” (Yeremia 31:10) Warekabu wanapewa ahadi kwa sababu nzuri. Yeremia anawekwa “kifungoni katika Ua wa Walinzi.” (Yeremia 37:21) Yerusalemu linaharibiwa, na wakaaji wengi wanapelekwa utekwani. Yeremia na mwandishi wake, Baruku, ni kati ya wale wanaobaki. Watu hao wenye woga wanaenda Misri hata ingawa wameonywa na Yeremia wasiende huko. Sura ya 46 mpaka ya 51 zina ujumbe wa Yeremia kwa mataifa.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha YeremiaMnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
-
-
YERUSALEMU LATEKETEA
Ni mwaka wa 607 K.W.K. Huo ni mwaka wa 11 wa ufalme wa Sedekia. Mfalme Nebukadneza wa Babiloni amelizingira jiji la Yerusalemu kwa miezi 18 sasa. Katika siku ya saba ya mwezi wa tano ya mwaka wa 19 wa utawala wa Nebukadneza, Nebuzaradani, mkuu wa walinzi, ‘anaingia,’ au kufika Yerusalemu. (2 Wafalme 25:8) Labda kutoka katika kambi yake iliyo nje ya kuta za jiji, Nebuzaradani anachunguza hali na kupanga hatua ya kuchukua. Siku tatu baadaye, katika siku ya kumi ya mwezi huo, ‘anaingia’ Yerusalemu. Naye analiteketeza jiji hilo.—Yeremia 52:12, 13.
Yeremia anaeleza kwa undani jinsi Yerusalemu lilivyoangushwa. Kwa hiyo, maelezo yake yanasababisha maombolezo au vilio. Maombolezo hayo yamo katika kitabu cha Biblia kinachoitwa Maombolezo.
-