-
Kaa Macho, Kama Yeremia AlivyofanyaMnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
-
-
5, 6. (a) Yehova anatumia jamii ya Yeremia jinsi gani leo? (b) Funzo letu litakazia nini?
5 Katika nyakati zetu, kwa upendo Yehova amewaandalia wanadamu kikundi cha Wakristo watiwa-mafuta ambao kwa njia ya mfano wanatenda kama walinzi wanaowaonya watu kuhusu hukumu yake juu ya ulimwengu huu. Kwa makumi ya miaka, jamii hiyo ya Yeremia imekuwa ikiwahimiza watu wakazie fikira nyakati tunamoishi. (Yer. 6:17)
-
-
Kaa Macho, Kama Yeremia AlivyofanyaMnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
-
-
10. Kwa nini inaweza kusemwa kwamba mabaki ya watiwa-mafuta wako ‘juu ya mataifa na falme’?
10 Akiwa “Mfalme wa mataifa,” Yehova alimwagiza Yeremia atangaze ujumbe wa hukumu kwa mataifa na falme. (Yer. 10:6, 7) Lakini mabaki ya watiwa-mafuta wako “juu ya mataifa na juu ya falme” katika njia gani? (Yer. 1:10) Kama nabii huyo wa zamani, jamii ya Yeremia imepewa mgawo na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima. Kwa hiyo, watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta wamepewa mamlaka rasmi ya kutangaza ujumbe wa hukumu ulimwenguni pote juu ya mataifa na falme. Wakiwa wamepewa mamlaka na Mungu Aliye Juu Zaidi na wakitumia lugha iliyo wazi ya Neno lake lililoongozwa na roho takatifu, jamii ya Yeremia inatangaza kwamba mataifa na falme za leo zitang’olewa na kuharibiwa kwa njia ya Mungu wakati wake barabara utakapofika. (Yer. 18:7-10; Ufu. 11:18) Jamii ya Yeremia imeazimia kutopunguza bidii katika kazi waliyopewa na Mungu ya kutangaza duniani pote ujumbe wa hukumu ya Yehova.
-