-
Utachagua Marafiki wa Aina Gani?Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
3. Sedekia alitaka nini kutoka kwa Yeremia, naye Yeremia alifanya nini?
3 Mara kadha wa kadha, Mfalme Sedekia alitafuta ushauri wa Yeremia kabla ya Yerusalemu kuharibiwa. Kwa nini? Mfalme huyo alitazamia kupata majibu yenye kutia moyo kuhusu wakati ujao wa utawala wake. Alitaka Yeremia atangaze kwamba Mungu ataingilia kati na kukomboa Yuda kutoka kwa maadui wake. Kupitia wajumbe, Sedekia alimsihi Yeremia: “Tafadhali muulize Yehova kwa ajili yetu, kwa sababu Nebukadreza mfalme wa Babiloni anapiga vita juu yetu. Labda Yehova atatutendea kulingana na kazi zake zote za ajabu, hivi kwamba [Nebukadreza] aondoke kwetu.” (Yer. 21:2) Mfalme huyo hakutaka kufuata mwongozo wa Mungu wa kujitia mikononi mwa Babiloni. Msomi mmoja alimfananisha Sedekia na “mgonjwa anayerudi kwa daktari tena na tena ili kuhakikishiwa kwamba atapona, lakini hataki kutumia dawa alizoandikiwa.” Namna gani Yeremia? Angeweza kumfurahisha Sedekia kwa kumwambia alichotaka kusikia. Kwa nini basi Yeremia hakubadili ujumbe wake na kujirahisishia mambo? Alikataa kufanya hivyo kwa sababu Yehova alikuwa amemwambia atangaze kwamba jiji la Yerusalemu litaanguka.—Soma Yeremia 32:1-5.
-
-
Utachagua Marafiki wa Aina Gani?Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
Yeremia hangeweza kukatiza kabisa ushirikiano wake na Sedekia; hata wakati ambapo Sedekia alikataa kufuata shauri la Mungu, bado ndiye aliyekuwa mfalme. Hata hivyo, haikumaanisha kwamba lazima Yeremia afuate maoni yaliyopotoka ya mfalme au kumpendeza. Ni kweli kwamba kama Yeremia angefanya jinsi mfalme alivyotaka, Sedekia angeweza kumpa zawadi nyingi na kumfaa kwa njia nyinginezo. Badala yake, Yeremia alikataa kushinikizwa kuwa rafiki ya Sedekia. Kwa nini? Kwa sababu Yeremia hakuwa tayari kulegeza msimamo ambao Yehova alikuwa amemwambia achukue.
-