-
Ukristo Waenea Miongoni mwa Wayahudi wa Karne Ya KwanzaMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Kutaniko la Yerusalemu na Wayahudi Walioishi Nje ya Palestina
Yakobo, ambaye alihudhuria pia mkutano huo ambapo habari kuhusu maeneo ilizungumziwa, alikuwa mwangalizi katika kutaniko la Yerusalemu. (Matendo 12:12, 17; 15:13; Wagalatia 1:18, 19) Kwenye Pentekoste mwaka wa 33 W.K., alijionea jinsi maelfu ya Wayahudi walioishi nje ya Palestina ambao walikuja Yerusalemu walivyoitikia habari njema na kubatizwa.—Matendo 1:14; 2:1, 41.
Tangu hapo na baadaye, Wayahudi wengi walikuja kwa ajili ya sherehe zilizofanywa kila mwaka. Jiji lilijaa watu kupita kiasi, na wageni walilazimika kukaa katika vijiji vilivyokuwa kwenye ujirani au kupiga kambi katika mahema. Zaidi ya kukutana na marafiki wao, kichapo Encyclopaedia Judaica kinaeleza kwamba wasafiri hao waliingia hekaluni ili kuabudu, kutoa dhabihu, na kujifunza Torati.
Bila shaka, Yakobo na washiriki wengine wa kutaniko la Yerusalemu walichukua nafasi hizo kuwahubiria Wayahudi hao walioishi nje ya Palestina. Huenda mitume walifanya hivyo kwa busara nyingi katika kipindi cha ‘mateso makubwa yaliyotokea juu ya kutaniko lililokuwa katika Yerusalemu’ kwa sababu ya kuuawa kwa Stefano. (Matendo 8:1) Kabla na baada ya tukio hilo, ripoti inaonyesha kwamba bidii ya Wakristo hao katika kazi ya kuhubiri iliendelea kuongezeka.—Matendo 5:42; 8:4; 9:31.
-
-
Ukristo Waenea Miongoni mwa Wayahudi wa Karne Ya KwanzaMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Pia, makumi ya maelfu ya watu walienda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya sherehe mbalimbali. Masimulizi kwenye Matendo 2:9-11 kuhusu Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K., yanaonyesha hivyo. Wasafiri wa Kiyahudi waliokuwapo walitoka Parthia, Umedi, Elamu, Mesopotamia, Kapadokia, Ponto, Asia, Frigia, Pamfilia, Misri, Libya, Roma, Krete, na Arabia.
-