-
Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na AkavumiliaMnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 1
-
-
Pia, Yosefu aliipeleka familia yake kwenye sherehe za kidini huko Yerusalemu. Ili kuhudhuria sherehe ya Pasaka iliyofanywa kila mwaka, huenda Yosefu alihitaji kusafiri kwa majuma mawili mwendo wa kilomita 113, ili kusherehekea pindi hiyo kisha wangerudi nyumbani.
-
-
Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na AkavumiliaMnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 1
-
-
Walikuwa na “Hangaiko la Akilini”
Yesu alipokuwa na umri wa miaka12, kama kawaida Yosefu aliipeleka familia yake huko Yerusalemu. Ulikuwa wakati wa sherehe ya Pasaka, na familia kubwa zilisafiri pamoja katika msafara mrefu wakipita kwenye maeneo ya mashambani yenye mimea na nyasi ndefu. Walipokaribia eneo lisilo na mimea karibu na jiji kuu la Yerusalemu, wengi walianza kuimba zaburi za sifa zilizojulikana sana. (Zaburi 120-134) Huenda jiji hilo lilikuwa limejaa mamia ya maelfu ya watu. Baadaye, familia na misafara yao walianza kurudi nyumbani. Wakiwa na mengi ya kufanya, huenda Yosefu na Maria walidhani kwamba Yesu alikuwa akisafiri pamoja na washiriki wengine wa familia yao. Baada tu ya kusafiri kwa mwendo wa siku moja kutoka Yerusalemu ndipo walipotambua jambo lenye kushtua—Yesu hakuwa pamoja nao!—Luka 2:41-44.
Walirudi kwa haraka mpaka Yerusalemu. Wazia jinsi walivyochanganyikiwa walipopita katika barabara za jiji hilo, huku wakiita jina la mwana wao. Mvulana huyo alikuwa wapi? Baada ya kutafuta kwa siku tatu, Yosefu alianza kujiuliza ikiwa alikuwa ameshindwa kabisa kutimiza mgawo mtakatifu aliopewa na Yehova? Mwishowe wakaenda hekaluni. Walipofika huko, waliingia katika chumba fulani ambamo wanaume wengi wenye elimu, waliojua Sheria walikuwa wamekusanyika huku kijana Yesu akiwa ameketi katikati yao! Wazia kitulizo ambacho Yosefu na Maria walipata!—Luka 2:45, 46.
Yesu alikuwa akiwasikiliza wanaume hao wenye elimu na kuuliza maswali mengi. Wanaume hao walishangazwa na ufahamu wa mtoto huyo na majibu yake. Hata hivyo, Maria na Yosefu waliduwaa. Kulingana na simulizi hilo, Yosefu hasemi chochote. Lakini maneno ya Maria yanaonyesha jinsi wote wawili walivyohisi: “Mtoto, kwa nini umetutendea hivi? Tazama, baba yako nami tumekuwa tukikutafuta tukiwa na hangaiko la akilini.”—Luka 2:47, 48.
Hivyo, kwa ufupi, Neno la Mungu linatuonyesha kihalisi hali ambazo wazazi hupitia. Wazazi wanaweza kupatwa na mkazo hata kama mtoto ni mkamilifu! Wazazi katika ulimwengu huu ulio hatari wanaweza kupatwa na “hangaiko la akilini” kwa kiwango kikubwa, lakini akina baba na mama wanaweza kufarijiwa kujua kwamba Biblia inaonyesha kuwa wazazi wanakabili hali ngumu.
Jambo la kupendeza ni kwamba Yesu alikuwa amebaki mahali pekee ambapo angejihisi akiwa karibu zaidi na Baba yake wa mbinguni, Yehova, huku akijitahidi kujifunza mambo mengi iwezekanavyo. Hivyo, aliwajibu wazazi wake kwa njia rahisi na kwa unyoofu: “Kwa nini mlilazimika kunitafuta? Je, hamkujua kwamba ni lazima niwe katika nyumba ya Baba yangu?”—Luka 2:49.
Bila shaka, Yosefu alifikiria maneno hayo tena na tena. Labda maneno hayo yalimfurahisha. Kwa kweli, alikuwa amejitahidi kumfundisha mwana wake mlezi ahisi hivyo kumwelekea Yehova Mungu. Akiwa bado mvulana, tayari Yesu alitambua maana ya neno “baba”—huenda alijua maana ya neno hilo hasa kwa kushirikiana na Yosefu.
-