Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 1. Ni katika njia gani sherehe za Waisraeli zinafanana na makusanyiko ya wilaya ya siku hizi?

      1 Yosefu, Maria, watoto wao, na watu wengine walienda Yerusalemu kwa ukawaida kuhudhuria sherehe za kila mwaka. Wakati wa sherehe hizo, wao na waabudu wengine walijitahidi kutofikiria matatizo yao na badala yake kuzingatia mambo ya kiroho yaliyokuwa muhimu zaidi maishani mwao. Sherehe hizo ziliwapa fursa ya kutafakari na kuzungumza kuhusu wema wa Yehova na Sheria yake. Makusanyiko ya wilaya yanayokuja yatatupa fursa kama hizo za kumwabudu Yehova kwa shangwe.

      2. Tunapaswa kufanya nini ili tujitayarishe kwa ajili ya kusanyiko la wilaya linalokuja?

      2 Uhitaji wa Kujitayarisha: Familia ya Yesu iliyoishi Nazareti ilihitaji kutembea umbali wa kilomita 200 hivi kwenda na kurudi kutoka Yerusalemu. Ingawa hatujui Yesu alikuwa na ndugu na dada wangapi, tunaweza kuwazia jitihada ambazo Yosefu na Maria walifanya ili kujitayarisha kwa ajili ya safari hiyo.

  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 3. Ni katika njia gani sherehe za Waisraeli ziliandaa fursa za kuwa na ushirika wenye kujenga?

      3 Ushirika Wenye Kujenga: Kwenye sherehe za Wayahudi, waabudu walipata fursa ya kufurahia ushirika wenye kujenga. Bila shaka, familia ya Yesu ilitazamia kwa hamu kukutana tena na marafiki zao wa muda mrefu. Pia walifurahia fursa ya kuanzisha urafiki na baadhi ya Wayahudi na wageuzwa-imani wengi ambao walihudhuria sherehe hizo au ambao walikuwa wakisafiri kwenda au kutoka Yerusalemu.

  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 5. Ni nini kitakachotusaidia kunufaika kikamili na programu?

      5 Wakati wa Kujifunza: Tangu alipokuwa mtoto, Yesu alitumia vipindi vya sherehe kujifunza kumhusu Baba yake wa mbinguni. (Luka 2:41-49)

  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 6. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu mavazi na mapambo yetu?

      6 Mavazi na Mapambo: Wafanyabiashara wasio Wayahudi wangeweza kuitambua kwa urahisi familia ya Yesu na waabudu wengine Wayahudi waliokuwa wakisafiri kwenda na kurudi kutoka kwenye sherehe, kwa sababu miisho ya nguo zao ilikuwa na upindo wenye nyuzinyuzi, ambao ulikuwa na uzi wa bluu juu yake. (Hes. 15:37-41)

  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 9. Tunaweza kuigaje uthamini wa familia ya Yesu kwa maandalizi ya kiroho ya Yehova?

      9 Sherehe za kale zilikuwa vipindi vya shangwe ambavyo Wayahudi waliotaka kujifunza mengi kumhusu Yehova walitazamia kwa hamu. (Kum. 16:15) Familia ya Yesu ilifurahi kujidhabihu ili kuhudhuria sherehe hizo na kunufaika kikamili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki