-
Nuru kwa MataifaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Yehova ‘Ateta’
4, 5. (a) Yehova anavamia Yerusalemu jinsi gani? (b) Kwa nini tunaweza kukata kauli kwamba ni idadi ndogo tu kwa kulinganishwa ambayo itauokoka uharibifu wa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K.? (Ona kielezi-chini.)
4 Katika mistari ile inayoumalizia unabii wa Isaya wenye kusisimua, Yehova anatoa maelezo dhahiri sana kuhusu matukio yatakayoelekeza kwenye siku ya hasira yake. Tunasoma hivi: “BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto. Kwa maana BWANA atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na BWANA watakuwa wengi.”—Isaya 66:15, 16.
5 Maneno hayo yanapasa kuwasaidia watu wa siku za Isaya wautambue uzito wa hali yao. Wakati unakaribia ambapo Wababiloni wenye kuleta hukumu ya Yehova watavamia Yerusalemu, huku magari yao ya kivita yakitifua vumbi kwa fujo kana kwamba ni upepo wa kisulisuli. Hicho kitakuwa kivumbi cha kutisha wee! Yehova atatumia wavamizi hao kutimiza hukumu zake mwenyewe zilizo motomoto juu ya Wayahudi “wote wenye mwili” wasio waaminifu. Itakuwa kana kwamba Yehova mwenyewe anapigana na watu wake. “Ghadhabu” yake haitarudi nyuma. Wayahudi wengi wataanguka wakiwa ‘wameuawa na Yehova.’ Mwaka wa 607 K.W.K., unabii huo unatimizwa.a
6. Ni mazoea gani yenye hatia yanayotukia katika Yuda?
6 Je, Yehova ana haki ya ‘kuteta’ kwa kuwapinga watu wake? Tena sana! Katika mazungumzo yetu ya kitabu cha Isaya, tumeona mara nyingi kwamba Wayahudi wameingilia sana ibada ya uwongo, huku ikidhaniwa kwamba eti wamejiweka wakfu kwa Yehova. Na Yehova hajawa kipofu muda huo, asiweze kuyaona matendo yao. Tunaona hivyo tena katika maneno yafuatayo ya unabii: “Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA.” (Isaya 66:17) Je, Wayahudi hao ‘wanajitakasa na kujisafisha’ ili wajitayarishe kwa ajili ya ibada safi? La, hasha. Badala ya hivyo, wanajihusisha katika desturi za utakaso wa kipagani katika bustani za pekee. Kisha wanakula kwa pupa nyama ya nguruwe na viumbe wengine walioonwa kuwa wachafu chini ya Sheria ya Kimusa.—Mambo ya Walawi 11:7, 21-23.
-
-
Nuru kwa MataifaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Watauona Utukufu Wangu”
8. (a) Yuda na hata Jumuiya ya Wakristo zitapatwa na jambo gani? (b) Mataifa ‘yatauona utukufu wa Yehova’ jinsi gani?
8 Je, Yehova anaziona hatia za Jumuiya ya Wakristo na mafundisho yake ya uwongo? Ebu yasome maneno ya Yehova yafuatayo, kama yalivyoandikwa na Isaya, uone utakata kauli gani: “Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu.” (Isaya 66:18) Licha ya kujua na kuwa tayari kuhukumu matendo ya wale wanaodai kuwa watumishi wake, anayajua hata mawazo yao na atayahukumu hayo pia. Yuda anadai kuwa anamwamini Yehova, lakini matendo yake ya kuabudu sanamu na mazoea ya kipagani yanakanusha dai lake. Raia zake ‘wanajitakasa’ bure kulingana na desturi za kipagani. Taifa hilo litafyekwa, tena peupe mbele ya jirani zake wanaoabudu sanamu. Majirani hao ‘watauona utukufu wa Yehova’ kwa maana ya kwamba watashuhudia matukio hayo kwa macho yao wenyewe na kulazimika kukubali kwamba neno la Yehova limetimia. Yote hayo yanatumikaje kuhusu Jumuiya ya Wakristo? Wakati jumuiya hiyo itakapofikia mwisho wake, wengi wa wale waliokuwa rafiki zake na waliofanya biashara pamoja naye watalazimika kusimama kando tu na kutazama wakiwa hoi wakati neno la Yehova linapotimizwa.—Yeremia 25:31-33; Ufunuo 17:15-18; 18:9-19.
-