-
Je, Utaokolewa Mungu Atendapo?Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
Kati ya wale waokokaji 97,000, baadhi yao waliuawa mara moja; wengine walifanywa watumwa. Yosefo asema hivi: “Wale wenye umri wa zaidi ya miaka kumi na saba walifungwa kwa pingu na kutumwa Misri ili kufanya kazi ngumu, huku watu wengi wakitolewa na Tito kwa mikoa ili kuangamia kwenye nyanja za michezo kwa kuuawa kwa upanga au kwa kuuawa na hayawani-mwitu.” Hata wakati ukaguzi huo ulipokuwa ukiendelea, wafungwa 11,000 walikufa njaa.
-
-
Je, Utaokolewa Mungu Atendapo?Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
10. Tumeelezaje Mathayo 24:22 wakati uliopita?
10 Wakati uliopita ilielezwa kwamba “mwili ambao ungeokolewa” ulirejezea Wayahudi waliookoka ile dhiki juu ya Yerusalemu katika 70 W.K. Wakristo walikuwa wamekimbia, kwa hiyo Mungu aliweza kuruhusu Waroma walete uharibifu wa upesi. Yaani, kwa sababu ya jambo la hakika kwamba “wachaguliwa” hawakuwa hatarini, siku za dhiki ziliweza kukatwa ziwe fupi, hilo likiruhusu sehemu fulani ya “mwili” wa Kiyahudi iokolewe. Ilihisiwa kwamba Wayahudi waliookoka walifananisha wale ambao wangeokoka dhiki kubwa inayokuja katika siku yetu.—Ufunuo 7:14.
11. Kwa nini yaonekana kwamba elezo hilo la Mathayo 24:22 lapaswa lifikiriwe tena?
11 Lakini, je, elezo hilo linapatana na yale yaliyotendeka katika 70 W.K.? Yesu alisema kwamba “mwili” wa kibinadamu ulitazamiwa ‘kuokolewa’ kutoka katika ile dhiki. Je, ungetumia neno ‘kuokolewa’ ili kufafanua wale waokokaji 97,000, unapofikiria jambo la hakika kwamba maelfu kati yao yalikufa upesi kutokana na njaa kali au yalichinjwa katika majumba ya michezo? Yosefo asema hivi kuhusu jumba moja la michezo, katika Kaisaria: “Idadi ya wale walioangamia katika mashindano pamoja na hayawani-mwitu au katika kupigana mmoja na mwenzake au kwa kuteketezwa wakiwa hai, ilipita 2,500.” Ingawa hawakufa katika mazingiwa, wao bila shaka ‘hawakuokolewa.’ Na je, Yesu angewaona kuwa sawa na wale waokokaji wenye furaha wa “dhiki kubwa” inayokuja?
-