-
“Imeandikwa”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
a Baadaye, mwanahistoria wa karne ya kwanza Yosefo, Farisayo aliyekuwa ametalikiana na mke wake, alidokeza kwamba talaka iliruhusika “kwa sababu yoyote ile (na wanaume wanadai kwamba kuna sababu nyingi).”
-
-
“Imeandikwa”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
16. Viongozi wa dini waliipotosha jinsi gani amri ya Musa kuhusu talaka, naye Yesu alisema nini?
16 Pia, viongozi wa dini walibuni njia za kisheria za kuikwepa Sheria ya Mungu. Kwa mfano, Sheria ilimruhusu mtu kumtaliki mke wake ikiwa angeona “kitu fulani kisichofaa” kwake, pengine tatizo zito lililoiletea aibu nyumba yake. (Kumbukumbu la Torati 24:1) Hata hivyo, kufikia siku za Yesu, viongozi wa dini walitumia sheria hiyo kuwa udhuru wa kumruhusu mwanamume kumtaliki mke wake kwa kila sababu, hata kwa kuunguza chakula!a
-