-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
4. Wakristo katika Smirna walipatwa na upinzani mwingi sana kutoka kwa nani, naye Yesu aliwaonaje wapinzani hao?
4 Yesu anataja hasa kwamba Wakristo katika Smirna wamechukuana na upinzani mwingi mikononi mwa Wayahudi wa kimnofu. Katika siku za mapema zaidi, wengi wa dini hii walipinga kwa dhati kuenea kwa Ukristo. (Matendo 13:44, 45, 14:19) Sasa, miongo michache tu baada ya Yerusalemu kuanguka, Wayahudi hao katika Smirna wanaonyesha roho ile ile ya kishetani. Si ajabu kwamba Yesu anawaona hao kuwa “sinagogi la Shetani”!a
-
-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
a Yapata miaka 60 baada ya Yohana kufa, Polycarp mwenye umri wa miaka 86 aliteketezwa mpaka kifo katika Smirna kwa sababu yeye hangeweza kukana itikadi yake katika Yesu. The Martyrdom of Polycarp, kitabu kinachoitikadiwa kuwa cha wakati ule ule mmoja na tukio hili, hutaarifu kwamba wakati kuni zilipokuwa zikikusanywa za kuteketeza yeye, “wale Wayahudi walikuwa na bidii kupita kiasi, kama ilivyo desturi yao, katika kusaidia katika hili”—hata ingawa kufishwa huko kulitukia katika “siku kubwa ya Sabato.”
-