-
Kutia Muhuri Israeli wa MunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
15. Kabla tu ya siku ya Bwana, wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walifikiri Wayahudi asilia wangefurahia nini baada ya Majira ya Mataifa kuisha?
15 Hata hivyo, je! Waisraeli asilia leo hawastahili kadiri fulani ya upendeleo wa pekee? Katika pindi iliyokuwa kabla tu ya siku ya Bwana, wakati wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walipokuwa wakigundua tena nyingi za kweli za msingi za Neno la Mungu, ilidhaniwa kwamba Majira ya Mataifa yakiisha, Wayahudi wangefurahia tena msimamo wenye kibali mbele za Mungu. Hivyo, kitabu cha C. T. Russell The Time Is at Hand (Buku 2 la Studies in the Scriptures), kilichotangazwa 1889, kilitumia Yeremia 31:29-34 kuhusu Wayahudi asilia, na kueleza: “Ulimwengu ni shahidi wa uhakika wa kwamba adhabu ya Israeli chini ya utawala wa wasio Wayahudi imekuwa ikiendelea tangu K.K. [607], kwamba ingali inaendelea, na kwamba hakuna sababu ya kutazamia mtengenezo mpya wa kitaifa upesi zaidi ya M.B. 1914, kile kikomo cha ‘nyakati saba’ zao—miaka 2520.” Ilielekea kwamba wakati huo Wayahudi wangepata urudisho wa kitaifa, na kwa wazi tazamio hilo lilitiwa uangavu 1917, wakati Julisho-Wazi la Balfour lilipoahidi kuunga mkono Uingereza kwa kufanya Palestina kuwa kao la kitaifa kwa ajili ya Wayahudi.
16. Ni jitihada gani walizofanya Mashahidi wa Yehova kufikia Wayahudi asilia wakiwa na ule ujumbe wa Kikristo, na kukawa na tokeo gani?
16 Kufuata vita ya kwanza ya ulimwengu, Palestina ikawa eneo chini ya usimamizi wa Uingereza, na njia ikafunguka Wayahudi warudi kwenye bara hilo. Katika 1948 Dola la kisiasa la Israeli lilitokezwa. Je! hiyo haikuonyesha kwamba Wayahudi walikuwa katika mstari wa kupata baraka za kimungu? Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova waliitikadi kwamba ilikuwa hivyo. Hivyo, katika 1925 walitangaza kitabu chenye kurasa 128, Comfort for the Jews. Katika 1929 walitoa buku lenye kuvutia la kurasa 360, Life, ambalo lilikusudiwa livutie Wayahudi na pia lilishughulika na kitabu cha Biblia cha Ayubu. Jitihada kubwa zilifanywa, hasa katika Jiji la New York, kufikia Wayahudi kwa huu ujumbe wa Kimesiya. Kwa furaha, watu wachache mmoja mmoja waliitikia, lakini Wayahudi kwa ujumla, kama babu zao wa karne ya kwanza, waliikataa ithibati ya kuwapo kwa Mesiya.
17, 18. Watumwa wa Mungu walikuja kuelewa nini kuhusu agano jipya na unabii wa Biblia wa urudisho?
17 Ilikuwa wazi kwamba Wayahudi, wakiwa taifa, hawakuwa yule Israeli aliyeelezwa katika Ufunuo 7:4-8 au katika unabii mwingine wa Biblia unaohusu siku ya Bwana. Wakifuata pokeo, Wayahudi waliendelea kuepuka kutumia jina la kimungu. (Mathayo 15:1-3, 7-9) Kikizungumzia Yeremia 31:31-34, kitabu Jehovah, kilichotangazwa na Mashahidi wa Yehova katika 1934, kilitaarifu hivi kwa mkataa: “Lile agano jipya halihusiani kwa vyovyote na wazao asilia wa Israeli pamoja na aina ya binadamu kwa ujumla, bali . . . lina mpaka kwa Israeli wa kiroho tu.” Unabii wa Biblia juu ya urudisho hauhusu wala Wayahudi asilia wala Israeli ya kisiasa, ambayo ni mshiriki wa Umoja wa Mataifa na ni sehemu ya ulimwengu ambao Yesu alizungumzia kwenye Yohana 14:19, 30 na 18:36.
-
-
Kutia Muhuri Israeli wa MunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi nikasikia hesabu ya wale ambao walitiwa muhuri, mia na arobaini na nne elfu, waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli: Kutoka kabila la Yuda elfu kumi na mbili walitiwa muhuri; kutoka kabila la Reubeni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Gadi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Asheri elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Naftali elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Manase elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Simeoni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Lawi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Isakari elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Zebuloni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Yosefu elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Benyamini elfu kumi na mbili walitiwa muhuri.”—Ufunuo 7:4-8, NW.
11. (a) Ni kwa nini lile rejezo kwa makabila 12 halingeweza kutumika kuhusu Israeli halisi, wa mnofu? (b) Ni kwa nini Ufunuo huorodhesha makabila 12? (c) Ni kwa nini hakuna kabila ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani katika Israeli wa Mungu?
11 Je! hii haingeweza kuwa inarejeza kwa Israeli halisi, wa mnofu? La, kwa kuwa Ufunuo 7:4-8 hutofautiana na ile orodha ya kawaida ya kikabila. (Hesabu 1:17, 47) Kwa wazi, orodha hii hapa si kwa kusudi la kutambulisha Wayahudi wa mnofu kwa makabila yao bali ni kuonyesha muundo wa kitengenezo kama huo kwa Israeli wa kiroho. Hili linasawazika. Wanapaswa waweko washiriki 144,000 wa hili taifa jipya—12,000 kutoka kila mojapo makabila 12. Hakuna kabila katika huyu Israeli wa Mungu ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani. Taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa wafalme, na taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa makuhani.—Wagalatia 6:16; Ufunuo 20:4, 6.
12. Ni kwa nini inafaa kwamba wale wazee 24 wanaimba mbele ya Mwana-Kondoo maneno ya ule wimbo wa Ufunuo 5:9, 10?
12 Ijapokuwa Wayahudi asilia na waongofu wa Kiyahudi walipewa fursa ya kwanza ili wachaguliwe kwa ajili ya kuwa Israeli wa kiroho, ni wachache tu wa taifa hilo walioitikia. Kwa hiyo Yehova aliwatolea mwaliko wale wasio Wayahudi. (Yohana 1:10-13; Matendo 2:4, 7-11; Warumi 11:7) Kama vile kwa habari ya Waefeso, ambao hapo kwanza walikuwa “wametenganishwa na dola la Israeli,” sasa watu wasio Wayahudi wangeweza kutiwa muhuri kwa roho ya Mungu na kuwa sehemu ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 2:11-13; 3:5, 6; Matendo 15:14) Basi, inafaa wazee 24 kuimba mbele za Mwana-Kondoo: “Kwa damu yako wewe ulinunua watu kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na kikundi cha watu na taifa, na wewe ulifanya wao kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao wanapaswa kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”—Ufunuo 5:9, 10, NW.
13. Ni kwa nini ilifaa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote”?
13 Kundi la Kikristo ni “jamii teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu.” (1 Petro 2:9, NW) Likichukua mahali pa Israeli asilia likiwa taifa la Mungu, linakuwa Israeli mpya ambaye ni “‘Israeli’ kikweli.” (Warumi 9:6-8; Mathayo 21:43, NW)a Kwa sababu hii, ilifaa kabisa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake ya kiuchungaji “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote,” yaani, kwa kundi la ulimwenguni pote la Wakristo wapakwa-mafuta ambalo baadaye hesabu yalo ingekuwa 144,000.—Yakobo 1:1, NW.
-