Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati Wazee Watakapokuwa Vijana Tena
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Aprili 1
    • wakati huohuo pia akampa ujumbe huu mzuri kutoka kwa Mungu: “Mwachilie [Ayubu] ili asishuke chini kuingia shimoni [kaburi]! Nimepata fidia! Nyama yake na iwe laini kuliko wakati wa ujana; na arudi kwenye siku za nguvu za ujana wake.” (Ayubu 33:24, 25) Hapana shaka kuwa maneno hayo yalimpa Ayubu matumaini makubwa. Haikuwa lazima aendelee kuteseka mpaka kifo. Kama Ayubu angetubu, Mungu angefurahi kukubali fidia kwa ajili yake na angemwondolea misiba.a

      Ayubu alikubali kwa unyenyekevu kurekebishwa, na alitubu. (Ayubu 42:6) Yehova alikubali fidia kwa ajili ya Ayubu na kuiruhusu ifunike kosa lake. Jambo hilo lilifanya iwezekane kwa Mungu kumbariki Ayubu na kumrudisha katika hali nzuri. Yehova “a[li]ubariki mwisho wa Ayubu baadaye kuliko mwanzo wake.” (Ayubu 42:12-17) Wazia kitulizo ambacho Ayubu alipata, wakati Mungu alipomwondolea ugonjwa wake mbaya na nyama yake ikawa “laini kuliko wakati wa ujana”! Hiyo ilikuwa mojawapo ya baraka nyingi alizopata.

      Fidia ambayo Mungu aliikubali kwa ajili ya Ayubu ilikuwa na manufaa kidogo, kwa kuwa Ayubu bado alikuwa mtu asiye mkamilifu na baadaye alikufa.

  • Wakati Wazee Watakapokuwa Vijana Tena
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Aprili 1
    • a Neno “fidia” ambalo limetumiwa hapa linamaanisha “kufunika.” Katika kisa cha Ayubu, huenda fidia ilikuwa dhabihu ya mnyama, ambayo Mungu angeikubali ili kufunika, au kufanya upatanisho kwa ajili ya kosa lake.—Ayubu 1:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki