Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 1. Ni katika njia gani sherehe za Waisraeli zinafanana na makusanyiko ya wilaya ya siku hizi?

      1 Yosefu, Maria, watoto wao, na watu wengine walienda Yerusalemu kwa ukawaida kuhudhuria sherehe za kila mwaka. Wakati wa sherehe hizo, wao na waabudu wengine walijitahidi kutofikiria matatizo yao na badala yake kuzingatia mambo ya kiroho yaliyokuwa muhimu zaidi maishani mwao. Sherehe hizo ziliwapa fursa ya kutafakari na kuzungumza kuhusu wema wa Yehova na Sheria yake. Makusanyiko ya wilaya yanayokuja yatatupa fursa kama hizo za kumwabudu Yehova kwa shangwe.

      2. Tunapaswa kufanya nini ili tujitayarishe kwa ajili ya kusanyiko la wilaya linalokuja?

      2 Uhitaji wa Kujitayarisha: Familia ya Yesu iliyoishi Nazareti ilihitaji kutembea umbali wa kilomita 200 hivi kwenda na kurudi kutoka Yerusalemu. Ingawa hatujui Yesu alikuwa na ndugu na dada wangapi, tunaweza kuwazia jitihada ambazo Yosefu na Maria walifanya ili kujitayarisha kwa ajili ya safari hiyo.

  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma ya Ufalme—2010 | Juni
    • 3. Ni katika njia gani sherehe za Waisraeli ziliandaa fursa za kuwa na ushirika wenye kujenga?

      3 Ushirika Wenye Kujenga: Kwenye sherehe za Wayahudi, waabudu walipata fursa ya kufurahia ushirika wenye kujenga. Bila shaka, familia ya Yesu ilitazamia kwa hamu kukutana tena na marafiki zao wa muda mrefu. Pia walifurahia fursa ya kuanzisha urafiki na baadhi ya Wayahudi na wageuzwa-imani wengi ambao walihudhuria sherehe hizo au ambao walikuwa wakisafiri kwenda au kutoka Yerusalemu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki