-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Walikabili Magumu Makali
Alipofikia umri wa miaka 17, Yosefu alikuwa na tatizo kubwa katika familia yake. Ndugu zake wakubwa walitambua kwamba Yakobo, baba yao, “alimpenda [Yosefu] kuliko ndugu zake wote.” Hivyo, “wakaanza kumchukia, nao hawakusema naye kwa amani.” (Mwanzo 37:4) Tunaweza kuwazia jinsi hali hiyo ilivyomletea Yosefu hangaiko na mkazo. Mwishowe, chuki ya ndugu zake iliongezeka sana hivi kwamba wakamuuza utumwani.—Mwanzo 37:26-33.
Alipokuwa mtumwa huko Misri, Yosefu alikataa kutongozwa na mke wa bwana wake. Akiwa amekasirika kwa kukataliwa, mwanamke huyo alimshtaki Yosefu kwa uwongo kwamba alijaribu kumlala kinguvu. Alitiwa “katika nyumba ya gereza,” ambapo ‘walitesa miguu yake kwa pingu na nafsi yake ikaingia katika vyuma.’ (Mwanzo 39:7-20; Zaburi 105:17, 18) Hilo lilikuwa jaribu lililoje! Kwa miaka 13 hivi, Yosefu alikuwa ama mtumwa au mfungwa kwa sababu ya kutendewa na wengine isivyo haki, kutia ndani washiriki wa familia yake mwenyewe.—Mwanzo 37:2; 41:46.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Acha Kinyongo na Uchungu
Kwanza, wanaume hao waaminifu walijiepusha na uchungu na kinyongo. Alipokuwa gerezani, Yosefu angeweza kwa urahisi kuwafungia ndugu zake kinyongo kwa kumsaliti, labda kwa kufikiria jinsi ambavyo angeweza kulipiza kisasi ikiwa angewaona tena. Tunajuaje kwamba Yosefu aliyapinga mawazo hayo mabaya? Ona jinsi alivyotenda alipopata nafasi ya kulipiza kisasi juu ya ndugu zake ambao walikuja Misri kununua chakula. Masimulizi yanasema: “[Yosefu] akajitenga nao, akaanza kulia. . . . Baada ya hayo Yosefu akatoa amri, nao [watumishi wake] wakavijaza kabisa vyombo vya [ndugu zake] nafaka. Pia, walipaswa kurudisha pesa za watu hao kwenye gunia la kila mmoja wao na kuwapa vyakula kwa ajili ya safari.” Baadaye, alipowatuma ndugu zake wamlete baba yao Misri, Yosefu aliwatia moyo kwa maneno haya: “Msigombane njiani.” Kwa maneno na matendo, Yosefu alionyesha kwamba hakuacha uchungu na kinyongo vitawale maisha yake.—Mwanzo 42:24, 25; 45:24.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Jitahidi Kadiri Uwezavyo Kulingana na Hali Yako
Jambo la pili tunaloweza kujifunza ni kutoacha hali zetu zituzuie kufanya mambo ambayo tungefanya chini ya hali za kawaida. Huenda tukahangaikia sana mambo tusiyoweza kufanya hivi kwamba tunasahau yale tunayoweza kufanya. Hivyo, hali zetu huanza kututawala. Hilo lingetokea kwa Yosefu. Badala yake, alijitahidi kadiri alivyoweza kulingana na hali yake. Alipokuwa mtumwa, Yosefu ‘alizidi kupata kibali machoni pa bwana wake naye akamtumikia siku zote hata akamweka juu ya nyumba yake.’ Yosefu alikuwa na mtazamo huohuo alipokuwa gerezani. Kwa sababu ya baraka za Yehova na bidii ya Yosefu, ‘ofisa mkuu wa nyumba ya gereza aliwatia mkononi mwa Yosefu wafungwa wote waliokuwa katika nyumba hiyo ya gereza; na yote waliyokuwa wakifanya humo yeye ndiye aliyekuwa akiagiza yafanywe.’—Mwanzo 39:4, 21-23.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Mngojee Yehova
Jambo la tatu la kujifunza ni kwamba badala ya kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kurekebisha hali zetu, tunapaswa kumngojea Yehova. Mwanafunzi Yakobo aliandika: “Acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yakobo 1:4) Tunapaswa kuacha uvumilivu “ukamilishe kazi yake” kwa kuvumilia majaribu hadi mwisho bila kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kuyakomesha upesi. Hivyo, imani yetu itajaribiwa na kusafishwa, na itafunuliwa kama imani yetu ina nguvu ya kututegemeza. Yosefu na Daudi walikuwa na uvumilivu wa aina hiyo. Hawakujaribu kutafuta suluhisho ambalo lingeweza kumkasirisha Yehova. Badala yake, walijitahidi kadiri walivyoweza kulingana na hali zao. Waliendelea kumngojea Yehova, nao wakapokea baraka nyingi sana kwa kufanya hivyo. Wote wawili walitumiwa na Yehova kuokoa na kuongoza watu wake.—Mwanzo 41:39-41; 45:5; 2 Samweli 5:4, 5.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Yehova Atakutegemeza
Tunaweza kunufaika kwa kutafakari jinsi watu wanaotajwa na Biblia, kama vile Yosefu na Daudi, walivyofanikiwa kushughulika na hali ngumu na zenye kukatisha tamaa. Ingawa habari kuwahusu zinaelezwa katika kurasa chache tu za Biblia, majaribu yao yalidumu kwa miaka mingi. Jiulize hivi: ‘Watumishi hao wa Mungu walijifunzaje kukabili hali zao? Walidumishaje shangwe yao? Walipaswa kukuza sifa gani?’
-