Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Baadhi ya watumishi wa Mungu leo wanakumbwa na magonjwa ya kudumu yenye kudhoofisha au mikazo ya kihisia. Akiwa na umri wa miaka 18, Magdalena, aligunduliwa kuwa ana ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili (systemic lupus erythematosus). Inaonekana kwamba katika ugonjwa huo, kinga ya mwili hushambulia viungo vya mwili. Magdalena anasema hivi: “Niliogopa sana, kadiri wakati ulivyopita ndivyo hali yangu ilivyozidi kudhoofika na hali ikawa mbaya zaidi kwa sababu ya matatizo ya kutomeng’enya chakula vizuri, vidonda vya mdomoni, na matatizo ya koo.” Kwa upande mwingine, Izabela, analazimika kukabiliana na hali ambazo hazionekani wazi. Anaeleza hivi: “Tangu utotoni nimekuwa nikikabiliana na hali ya kushuka moyo. Hilo limesababisha nishikwe na hofu za ghafla, matatizo ya kupumua, na maumivu ya tumbo. Matokeo yake ni kwamba kwa kawaida ninahisi nikiwa mchovu.”

      Kukabiliana na Hali

      Magonjwa na udhaifu mbalimbali unaweza kubadili kabisa maisha yako. Hilo linapotokea, ni vizuri kutulia na kuichanganua hali yako kwa unyoofu. Huenda isiwe rahisi kukubali udhaifu ulionao. Magdalena anasema hivi: “Ugonjwa nilionao unazidi kuwa mbaya. Mara kwa mara ninajihisi nimechoka sana nisiweze kutoka kitandani. Kwa sababu ya hali isiyotabirika ya ugonjwa wangu, ni vigumu sana kupanga mambo ya baadaye. Jambo linalonivunja moyo sana ni kwamba siwezi tena kufanya mengi katika utumishi wa Yehova kama nilivyokuwa nikifanya zamani.”

      Zbigniew anaeleza hivi: “Kadiri miaka inavyozidi kupita, ndivyo ugonjwa wa yabisi-kavu unavyofanya niishiwe na nguvu hata zaidi, ukiharibu kiungo kimoja baada ya kingine. Nyakati nyingine, maumivu yanapokuwa makali sana, siwezi kufanya hata kazi ndogo tu. Hilo hunivunja moyo sana.”

      Miaka kadhaa iliyopita, Barbara aligunduliwa kuwa ana uvimbe uliozidi kukua kwenye ubongo. Anaeleza hivi: “Mwili mwangu umebadilika ghafula. Ninahisi nimelegea, kichwa kinaniuma mara kwa mara, na ninashindwa kukaza uangalifu. Kwa sababu ya hali hiyo mpya, nililazimika kupanga upya kila jambo.”

      Watu hao wote ni watumishi waliojiweka wakfu wa Yehova. Kufanya mapenzi ya Yehova ndilo jambo kuu katika maisha yao. Wanamtegemea Mungu kabisa na wananufaika kutokana na utegemezo wake.—Met. 3:5, 6.

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Kwa kumtegemea Mungu kupitia sala, Magdalena anaendelea kukabiliana na ugonjwa wake wenye kudhoofisha. Anasema hivi: “Kumweleza Yehova yaliyo moyoni mwangu hunituliza na kunirudishia shangwe yangu. Kwa kweli, sasa ninaelewa kumtegemea Mungu siku kwa siku kunamaanisha nini.”—2 Kor. 1:3, 4.

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Barbara anasema hivi kuhusu binti yake na dada wengine vijana katika kutaniko: “Wananisaidia ili nishiriki katika huduma. Bidii yao inanichangamsha.” Zbigniew huona utegemezo anaopata kutoka kwa mke wake kuwa wenye thamani kubwa. “Yeye hushughulikia karibu kazi zote za nyumbani. Pia, yeye hunisaidia kuvaa nguo na mara nyingi ananibebea mkoba wangu tunapoenda katika mikutano ya Kikristo na katika huduma.”

      Waamini wenzetu: Tunaposhirikiana na waamini wenzetu, tunatiwa moyo na kufarijiwa. Lakini vipi ikiwa huwezi kuhudhuria mikutano kwa sababu ya ugonjwa wako? Magdalena anaeleza hivi: “Kutaniko limehakikisha kwamba ninafaidika na mikutano kwa kunirekodia mikutano. Mara kwa mara waamini wenzangu hunipigia simu ili kujua jinsi wanavyoweza kunisaidia. Pia, wao hunitumia kadi zinazotia moyo. Kujua kwamba ndugu na dada wananikumbuka na kujali hali yangu hunisaidia kuendelea kuvumilia.”

      Izabela, ambaye ana ugonjwa wa kushuka moyo, anaeleza hivi: “Nina ‘baba’ na ‘mama’ wengi katika kutaniko, wale wanaonisikiliza na kujitahidi kunielewa. Kutaniko ni familia yangu—hapa ndipo ninapopata amani na shangwe.”

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Magdalena anasema hivi: “Ninajitahidi sana ili nisiyakazie fikira matatizo yangu. Mimi hujitahidi kufurahia siku ambazo ninajihisi vizuri. Ninatiwa moyo sana ninaposoma masimulizi ya maisha ya watu ambao wamebaki wakiwa waaminifu licha ya magonjwa yao ya kudumu.” Izabela anaimarishwa kwa kujua kwamba Yehova anampenda na kumthamini sana. Anasema hivi: “Ninahisi kwamba ninahitajika, na kwamba nina mtu ambaye ninaweza kutumia maisha yangu kwa ajili yake. Pia, nina tumaini zuri ajabu la wakati ujao.”

      Zbigniew anasema hivi: “Ugonjwa wangu unanifundisha kuwa mnyenyekevu na mtiifu. Unanifundisha kuonyesha ufahamu na hivyo kufanya maamuzi ya busara na pia kusamehe kutoka moyoni. Nimejifunza kufurahia kumtumikia Yehova bila kujisikitikia. Kwa kweli, nimechochewa kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki