-
Shangilieni Pamoja na Mungu Mwenye FurahaMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
4, 5. (a) Yehova alihisije wanadamu wa kwanza walipoasi? (b) Yehova alidumishaje mtazamo mzuri kuelekea wanadamu?
4 Katika bustani ya Edeni, Adamu na Hawa walikuwa na afya nzuri na akili kamilifu. Waliishi katika mazingira mazuri na walikuwa na kazi yenye kuthawabisha. Zaidi ya yote, walikuwa na pendeleo la kuwasiliana na Yehova kwa ukawaida. Mungu alikusudia wawe na wakati ujao wenye furaha. Lakini wazazi wetu wa kwanza hawakuridhika na zawadi hizo nzuri; waliiba tunda lililokatazwa kutoka katika “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Tendo hilo la kutotii lilisababisha hali ya huzuni ambayo sisi wazao wao hupatwa nayo leo.—Mwanzo 2:15-17; 3:6; Waroma 5:12.
5 Hata hivyo, Yehova hakupoteza shangwe yake kwa sababu ya mtazamo wa Adamu na Hawa wa kukosa shukrani. Alikuwa na uhakika kwamba baadhi ya wazao wao wangechochewa na mioyo yao kumtumikia. Alikuwa na uhakika mwingi sana hivi kwamba hata kabla Adamu na Hawa hawajapata mtoto wao wa kwanza, alitangaza kusudi lake la kukomboa wazao wao watiifu! (Mwanzo 1:31; 3:15) Katika karne zilizofuata, wengi walitenda kama Adamu na Hawa, lakini Yehova hakuwakataa wanadamu kwa sababu ya kutotii huko kulikoenea sana. Badala yake, alielekeza fikira zake kwa wanaume na wanawake ‘walioufurahisha moyo wake,’ wale waliojitahidi kwelikweli kumpendeza kwa sababu walimpenda.—Mithali 27:11; Waebrania 6:10.
-
-
Shangilieni Pamoja na Mungu Mwenye FurahaMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
8. Taja baadhi ya njia ambazo twaweza kumwiga Yehova na Yesu katika kudumisha shangwe yetu.
8 Bila shaka, sote twaweza kunufaika kwa kuiga mfano uliowekwa na Yehova Mungu na Kristo Yesu kuhusu jinsi ya kudumisha shangwe. Je, twaweza kumwiga Yehova kwa ukamili zaidi labda kwa kutokuwa na wasiwasi kupita kiasi mambo yasipotukia kama tulivyotarajia?
-